LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 10, 2021

UFARANSA KUTOA SH. BILIONI 413 KWA AJILI YA AWAMU YA TANO YA KUENDELEZA MRADI WA MABASI YA MWENDOKASI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimuelezea jambo Balozi wa Ufaransa hapa nchini, Frederic Clavier, wakati walipokutana na kuzungumza katika Ofisi ndogo za Wizara hiyo jijini Dar es Salaam, leo.


Dar es Salaam

Serikali ya Ufaransa imeahidi kutoa Euro milioni 150 sawa na Sh. Bilioni 413 kwa ajili ya kuendeleza mradi wa awamu ya tano wa ujenzi wa mradi wa mabasi ya mwendokasi jijini Dar es Salaam.


Ahadi hiyo imetolewa na Balozi wa Ufaransa hapa nchini, Frederic Clavier wakati  mazungumzo yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi, (Mb) katika Ofisi Ndogo za Wizara hiyo jijini Dar es Salaam, leo.


Prof. Kabudi amesema kuwa mazungumzo yake na Clavie yalijikita katika utekelezaji wa mambo waliyokubaliana wakati alipofanya ziara ya kikazi mwezi Februari mwaka huu, nchini Ufaransa

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages