LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 14, 2021

MGOGORO WA ARDHI ENEO LA CHASIMBA, CHACHUI ,CHATEMBO PAMOJA NA KIWANDA CHA SARUJI CHA WAZO WAFIKIA TAMATI

 

      

***************************************************

Mgogoro huo wa kiwanja chenye ukubwa wa hecta 224.8 uliodumu kwa takribani Miaka Saba ukihusisha wananchi wapatao 4000 kutoka cha simba, chatembo, chachui pamoja na kiwanda cha saruji cha Wazo umemalizika leo.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya Waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mhe.William lukuvi kukutana na wananchi katika mkutano wa hadhara na kutoa mapendekezo yaliyofikiwa katika mazungumzo ya muda mrefu kati ya Serikali na bodi ya kiwanda cha saruji kuhusiana na mstakabali wa wananchi katika eneo ambalo thamani yake ni takribani bilioni 60 za kitanzania.

Amesema ” Leo tunabadilisha historia ya kuitwa wavamizi , na kuwa wamiliki halali baada ya kila mmoja wenu kutimiza wajibu wake unaompasa ndani ya miezi sita kuanzia Sasa, utakaompa kila mwananchi haki ya kumiliki kihalali baada ya taratibu zote za umilikishwaji kukamilika. Hii ndio Serikali ya Dr.John Pombe Joseph Magufuli inayojali wananchi wanyonge” Mhe. William Lukuvi..

Aidha amesisitiza kuwa lengo la Serikali si kuingilia muhimili wa mahakama, bali ni kutafuta suluhu yenye lengo la kunufaisha pande zote mbili kwa mstakabali wa nchi yetu.

Ameongeza kuwa kukamilika kwa wajibu wa kila mwananchi kutafuatiwa na taratibu za umilikishwaji wa ardhi kihalali na upatikanaji wa maeneo muhimu kama vile maeneo ya makazi, biashara, huduma za Jamii, maeneo ya shule, zahanati, ofisi chekechea, makanisa na masoko.

Katika hatua nyingine Mhe. Lukuvi ameruhusu Manispaa ya Kinondoni kupeleka huduma muhimu za Jamii Kama vile shule, zahanati, vituo vya afya pamoja na kuboresha mtandao wa barabara utakaowarahisishia wananchi hao katika shughuli zao za kila siku.

Mkutano huo umehudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wakiwemo wa vyama na Serikali kwa lengo la kuongeza nguvu ya pamoja Katika kuhakikisha Sera ya Serikali ya awamu ya tano ya kutetea wanyonge inatekelezwa.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages