LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 30, 2021

DK. MPANGO KUAPISHWA KEHO KUWA MAKAMU WA RAIS, IKULU, JIJINI DODOMA

Dk. Philip Mpango


Ikulu, Chamwino.

Makamu wa Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Philip Isdor Mpango ataapishwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Taarifa iiyotolewa na Ikulu jijini Dodoma, imsema, Mpango ataapishwa katika Hafla itakayofanyika Ikulu, Chamwino jijini Dodoma kuanzia saa 9:00 alasiri na itaonyeshwa moja kwa moja na vyombo vya habari vya redio, televisheni na mitandao ya kijamii


Dk. Mpango ataapishwa kushika wadhifa huo baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kuwasilisha mapendekezo ya jina la Dk. Philip Isdor Mpango kuwa Makamu wa Rais katika Kikao Maalum cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi na baadaye jina hilo kuwasilishwa Bungeni na kupitishwa kwa asilimia 100 ya kura

Bungeni 

Akitangaza matokeo baada ya wbunge kupiga kura leo za kumthibitisha Dk. Mpango kuwa Makamu wa Rais, Spika wa Bunge Job Ndugai alisema kuwa jina la Dk. Mpango limethibitishwa kwa asilimia 100 kwani wabunge waliopiga kura ni 363 na sasa anasubiri kuapishwa na Jaji Mkuu.

"Wabunge waliokuwepo humu ndani ni 363 na wote wamepiga kura ya ndio kuthibitisha jina la Dk.Philip Mpango kuwa Makamu wa Rais mteule wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Hivyo amethibitishwa kwa asilimia 100 ya kura ambazo zimemthibitisha.Kwa mujibu wa Katiba anasubiri kuapishwa," alisema Ndugai.

Alisema baada ya jina lake kuthibitishwa na Bunge, Katiba inaweka wazi kwamba jimbo la Buhigwe sasa liko wazi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi itaendelea na mchakato wa kutangaza rasmi ratiba ya uchaguzi mdogo kwa ajili ya kujaza nafasi hiyo ambayo imeachwa wazi baada ya Dk.Mpango jina lake kuthibitishwa na Bunge kuwa Makamu wa Rais.

Kabla ya kutangaza matokeo hayo, Spika Ndugai alimpa nafasi Dk.Mpango ya kuzungumza kwa mara mwisho ndani ya Bunge hilo kwani baada ya hapo hataruhusiwa kuzungumza chochote kwa mujibu wa Katiba.

Kabla ya kumkaribisha Dk. Mpango, Spika Nduga aliwaambia wabunge kwa mujibu wa Katiba jina lake likashapitishwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hataweza kuzungumza bungeni, hivyo ni vema akazungumza kabla ya jina kuthibitishwa na Bunge.

"Nimehangaika sana kupata jibu la nini tufanye, nimeangalia katiba yetu inaeleza wazi kabisa, hivyo tukisubiri athibitishwe na Bunge kisha aseme haitawezekana, hivyo azungumze kabla jina halijathibitishwa.Kuna watu huko nje huko wataanza kusema Spika hakufuata Katiba.Dk.Mpango karibu uzungumze na wabunge kwa mara mwisho humu ndani,"alisema Spika Ndugai.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages