LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 16, 2021

WAZIRI NDUGULILE AFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU MKUU WA UMOJA WA POSTA AFRIKA


Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt Faustine Ndugulile  akizungumza na waandishi wa habari  akiwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Posta Afrika, Younouss Djibrine ofisini kwake Mtumba Jijini Dodoma  leo Februari 16,2021 ambaye wamekutana kuzungumzia uboreshaji wa huduma za Posta hapa nchini. 

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt Faustine Ndugulile  akizungumza na waandishi wa habari  akiwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Posta Afrika, Younouss Djibrine (kulia) ofisini kwake Mtumba Jijini Dodoma  leo Februari 16, 2021 ambaye wamekutana kuzungumzia uboreshaji wa huduma za Posta hapa nchini. kushoto Katibu Mkuu wizara hiyo Dkt Zainabu Chaula.


Ndugulile akiteta jambo na mgeni wake
Wanahabari wakiwa kazini wakati wa tukio hilo.



Na Richard Mwaikenda, CCM Blog, Dodoma

 WAZIRI wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile leo amekutana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mashirika ya Posta Afrika (PAPU), Younouss Djibrine na kufanya naye mazungumzo kwenye ofisi ya wizara hiyo katika Mji wa Kiserikali wa Mtumba, jijini Dodoma.

Pamoja na mambo mengine Katibu Mkuu amesema kuwa  nia ya kukutana naye ni kumpongeza Waziri Ndugulile kwa kuteuliwa na Rais John Magufuli kushika wadhifa huo mpya pamoja na kumueleza hatua iliyofikiwa ya maendeleo ya ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Umoja wa Posta Afrika jijini Arusha.Jengo hilo linajengwa kwa ushirikiano wa PAPU na Serikali ya Tanzania.


Aidha, Waziri Ndugulile amesema kuwa  pamoja na mambo mengine wamekubaliana na Katibu Mkuu huyo wa PAPU namna bora ya kuziendesha huduma za posta na namna ya kuboresha huduma za posta katika kuziendesha kidigitali na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya Sayansi na teknolojia.

Mdau nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video yaliyojiri kwenye kikao hicho wakati Waziri Ndugulile na Katibu mkuu wa PAPU, Djibrine wakizungumza na vyombo vya habari leo Februari 16...
IMEANDALIWA NA: RICHARD MWAIKENDA
 MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM
 0754264203

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages