LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 19, 2020

MWILI WA BABA MZAZI WA DC JOKATE MWENGELO, ALIYEFARIKI LEO KUZIKWA JUMANNE IJAYO MBINGA MKOANI RUVUMA

Mazishi ya Baba Mzazi wa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo, Mzee Urban Costa Ndunguru (Pichani), ambaye amefariki leo alfajiri katika Hospitali ya Taifa Muhimbili yanatarajiwa kufanyika Jumanne December 22, 2020, katika kijiji cha Tanga, Mbinga mkoani Ruvuma.


Taarifa zimesema, mwili wa marehemu unatarajiwa kuagwa keshotwa Jumatatu December 21, 2020 katika Kanisa la St Peters DSM, kisha kusafirishwa Jumatatu hiyo hiyo kwenda Mbinga Mkoani Ruvuma kwa ajili ya mazishi hayo.


Kabla ya kifo chake Mzee Urban Costa Ndunguru aliwa amelazwa amelazwa (ICU) kwa muda sasa baada ya kupata kiharusi (stroke).

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages