LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 23, 2020

METACHA MNATA AOKOA PENALTI DAKIKA YA MWISHO, YANGA SC YATOA SARE 1-1 NA NAMUNGO DAR

 

Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM

MLINDA mlango, Metacha Boniphace Mnata leo ameinusuru klabu yake, Yanga SC kupoteza mechi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuokoa mkwaju wa penalti wa dakika ya mwisho wa Mrundi, Bigirimana Blaise timu hiyo ikitoa sare ya 1-1 na Namungo FC ya Ruangwa mkoani Lindi.

Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam, Mnata aliuchupia mkwaju huo na kuupangua kabla ya kuuondosha hatarini na kuamsha shangwe za mashabiki wa timu ya Jangwani – wakishukuru kwa sare ya nyumbani kuliko kupoteza mechi.

Penalti hiyo ilitolewa na refa Raphael Ikambi kutoka Morogoro baada ya beki muhimili wa safu ya ulinzi ya Yanga, Bakari Nondo Mwamnyeto kumuangusha winga wa Namungo FC, Shiza Ramadhani Kichuya kwenye boksi. 

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages