LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 12, 2020

MKUU WA MKOA WA RUVUMA CHRISTINA MNDEME ACHANGIA KANISA TANI TANO ZA SARUJI

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme akizungumza katika Maadhimisho ya kutimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa Kanisa la Menonite  mjini Songea mkoani Ruvuma.

Na Mwandishi Maalum Ruvuma

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme  amewaomba viongozi wa Dini kuoimbea amani Tanzaniai kuelekea uchaguzi  mkuu uliopagwa kufanyika Siku ya Jumatano, Oktoba 28,2020.


Mndeme ametoa ombi hilo katika Maadhimisho ya kutimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa Kanisa la Menonite  mjini Songea mkoani Ruvuma, ambapo pamoja na ombi hilo,  alichangia tani tano za sariji yenye thamani ya sh. milioni 1.5 kwa ajili ya Ujenzi wa Kanisa hilo.


“Endeleeni kuiombea nchi yetu, tunasali hapa kwa sababu kuna amani  wengine wanakimbia na masanduku na watoto  kwa sababu hakuna amani katika nchi zao”, alisisitiza Mndeme.


Mndeme amewaomba wananchi wa Mkoa wa Ruvuma na Watanzania kwa ujumla kuendelea  kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli pamoja na wasaidizi wake ili nchi ya Tanzania ipate maendeleo zaidi katika sekta mbalimbali.


Kwa upande wake Mchungaji wa Kanisa la Moroviani Usharika wa Songea mjini Selemani Nzyemba akizungumza kwa niaba ya Mchungaji wa Kanisa la Menonite amemshukuru Mkuu wa Mkoa na timu yake kwa kwa msaada wa vifaa vya ujenzi.


Amesema msaada huo ni mkubwa kwa kanisa hilo ambao utasaidia kuendeleza ujenzi na kwamba pia amemshukuru kwa kuacha majukumu yake na kufika kushiriki katika  ibada ya kuazimisha mwaka mmoja tangu kuanzisha kanisa hilo mjini Songea.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages