LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 22, 2020

WAHARIRI UNGENI MKONO SUALA LA BIMA YA AFYA KWA WOTE- KONGA


Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bernard Konga akizungumza maneno ya utangulizi wakati wa Mkutano wa Tano na Wahari wa Vyombo vya Habari nchini jijini Dodoma Oktoba 22, 2020 kuelekea maadhimisho ya miaka 20 tangu mfuko huo uanzishwe rasmi 2001.





Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Edward Mbanga akizungumza alipokuwa akifungua mkutano wa majadiliano na wahariri wa vyombo vya habari nchini,  kuhusu uboreshaji wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kuelekea miaka 20 ya mfuko huo  jijini Dodoma Oktoba 22, 2020. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA.

 

Mkurugenzi wa Huduma za Wanachama wa NHIF, Christopher Mapunda  akielezea utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya NHIF, mafanikio na utatuzi wa changamoto mbalimbali kuelekea maadhimisho ya miaka 20 ya  mfuko huo.
Mhariri wa Kituo cha Televisheni/Radio CLOUDS, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Joyce Shebe akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wahariri wakati wa mkutano huo.
Meneja Uhusiano wa NHIF, Joyce Mziray akiongoza mkutano huo.

Selina Wilson wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo   akichangia mada wakati wa mkutano huo.

 Joseph Mwendapole kutoka gazeti la Nipashe, akiuliza swali na kutoa ushauri kwa NHIF kwa lengo la kuuboresha mfuko huo muhimu kwa afya ya jamii.


            Noor Shija kutoka Gazeti la Mwananchi Dodoma,

Leonard Mwakalebela wa Gazeti la Daily News, 

Mhariri kutoka gazeti la Habari Leo, Stellah Nyemenohi



Manyerere Jackton wa gazeti la  Jamhuri.

John Daniel wa gazeti la Raia Mwema

Mgeni Rasmi, Edward Mbanga na Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernard Konga  pamona na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini.









Meneja Uhusiano wa NHIF, Mziray akitoa maelekezo kuhuu uendeshaji wa mkutano huo.

Wahariri wakisikiliza kwa makini wakati wa mkutano huo.





Na Richard Mwaikenda.

MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bernard Konga amewaomba wahariri wa vyombo vya habari nchini, kuunga mkono agenda ya serikali kuwa na muswada wa kutungwa kwa sheria ya Bima ya Afya kwa Wote.

Ombi hilo alilitoa wakati wa mkutano wa tano na wahariri wa vyombo vya habari nchini uliofanyika Oktoba 22, 2020  jijini Dodoma.

Konga alisema vyombo vya habari ni muhimu sana katika kuelimisha jamii, hivyo ametaka uwepo ushirikiano kuhakikisha suala hilo linafanikiwa kwa kiwango kikubwa ili watanzania wote wawe na Bima ya Afya.

Pia amewasihi wahariri kushiriki kutoa maoni na ushauri  wa kuboresha upatikanaji wa huduma kwa wanachama na Umma kwa ujumla, Kuendelea kuwa mabalozi wa Mfuko kupitia Taaluma zao.

Wameshauriwa kutumia Ofisi za Mfuko zaidi ya 30 katika mikoa ili kutatua changamoto zinazojitokeza kwa wanachama, lakini pia kujenga ushirikiano na Mfuko katika kutoa elimu kwa wanachama na umma kwa ujumla kuhusu dhana na umuhimu wa bima ya afya. 

Katika mkutano huo uliofunguliwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Bernard Mbanga, wahariri wameshiriki majadiliano na kutoa ushauri mbalimbali jinsi ya kuboresha huduma za mfuko huo ambao mwakani unaadhimisha mika 20 tangu uanzishwe rasmi 2001.








No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages