LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 9, 2020

BENKI YA I&M YASHEREHEKEA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA

 

 Wafanyakazi wa I&M Benki wakisherehekea pamoja na wateja maadhimisho ya wiki ya wateja huku wakiwa katika mavazi ya utamaduni ambapo siku ya Jumatano oktoba 7 ndio maadhimisho rasmi ya utamaduni wa Afrika.
Wafanyakazi wa I&M Benki wakisherehekea pamoja na wateja maadhimisho ya wiki ya wateja huku wakiwa katika mavazi ya utamaduni ambapo siku ya Jumatano oktoba 7 ndio maadhimisho rasmi ya utamaduni wa Afrika.
Wafanyakazi wa I&M Benki wakisherehekea pamoja na wateja maadhimisho ya wiki ya wateja huku wakiwa katika mavazi ya utamaduni ambapo siku ya Jumatano oktoba 7 ndio maadhimisho rasmi ya utamaduni wa Afrika.

Wafanyakazi wakiwa pamoja na wateja wa benki ya I&M siku ya Jumaatano ambapo benki hiyo iliadhimisha kilele cha Wiki ya Huduma kwa Wateja kwa kukata keki na wateja wao waliotembelea benki siku hiyo. Licha ya kukata keki pia benki ilichukua fursa ya kutembelea wateja wa kila ngazi, kutoa zawadi kama shukrani kwa wateja pamoja na kuvaa mavazi ya aina mbalimbali kuonyesha utofauti na furaha ya kuhudumia 

Wafanyakazi wa Benki ya I&M wakitoa zawadi kwa mteja wa benki hiyo kama moja ya njia ya kuwashukuru wateja kwa kuendelea kuitumia na kuiamini Benki ya I&M kwa huduma bora inazotoa kwa wateja wake na jamii kwa ujumla.


Wafanyakazi wa I&M Benki wakisherehekea pamoja na wateja maadhimisho ya wiki ya wateja huku wakiwa katika mavazi ya utamaduni ambapo siku ya Jumatano oktoba 7 ndio maadhimisho rasmi ya utamaduni wa Afrika.
Wafanyakazi wa Benki ya I&M wakiwa katika mavazi ya udaktari wakionyesha kuwapatia wateja suluhisho la changamoto za kifedha kwa kuwapatia wateja huduma bora kibenki ili kufanikisha shughuli za kibiashara na uchumi. Haya yote yamefanyika katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja 

Wafanyakazi wa Benki ya I&M wakiwa katika mavazi ya udaktari wakionyesha kuwapatia wateja suluhisho la changamoto za kifedha kwa kuwapatia wateja huduma bora za kibenki ili kufanikisha shughuli za kibiashara na uchumi. Haya yote yamefanyika katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja 
Mfanyakazi wa Benki ya I&M katika mavazi ya udaktari akiwa anatoa huduma kwa mmoja kati ya wateja waliotembelea tawi la benki hiyo katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja
 

                                                      ...........................................

Dar es Salaam

BENKI ya I&M Tanzania imeadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja, kwa kutambua mchango muhimu unaotolewa na fanyakazi wake katika kuwahudumia wateja wao kwa viwango vya juu na kuhakikisha kuwa wanakuwa wenye furaha wakati wote.

Hafla hiyo ilifanyika leo maktaba square  jijini Dar es Salaam katika makao makuu ya benki hiyo, ikiambatana na shughuli mbalimbali kwa wateja kama ishara ya shukrani kwa wateja wanaothaminiwa na pia wafanyakazi wake ambao wamekuwa wakitekeleza jukumu muhimu la kutoa huduma bora kwa wateja wakati wote.

Miongoni mwa shughuli za kusherehesha hafla hiyo na wiki ya huduma kwa wateja zilizofanywa na benki hiyo ni pamoja na Maofisa wa juu na waandamizi wa benki hiyo akiwamo Afisa Mtendaji  Mkuu, walichukua jukumu la kuhudumia wateja katika matawi mbalimbali kwa siku ya leo.

Sheherehe hiyo ya wiki nzima ni matokeo ya kujitolea kwa benki hiyo ya I&M katika kuongeza ushiriki wa wafanyakazi katika kuunga mkono kaulimbiu ya mwaka huu ya siku hiyo inayosema kuwa, ‘Timu ya ndoto’.

Mbali na ushiriki wa watendaji wakuu, maafisa waandamizi katika kufanya jukumu la huduma kwa wateja, pia wafanyakazi wote wa benki hiyo walipokea barua binafsi za shukurani kwa bidii yao na kujitolea kwao katika kuleta matokeo chanya na furaha kwa wateja katika benki hiyo.

Mkuu wa Mauzo ya rejareja wa benki hiyo, Lilian Mtali alisema katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja wanataka onyesha thamani ya watoa huduma kwa wateja.

“Sisi benki ya I&M tunataka kutumia wiki hii ya huduma kwa wateja kuhakikisha kuwa tunawaonyesha thamani na ukarimu wateja wetu,lakini pia kuunga mkono na kutambua kazi nzuri na kubwa inayofanywa na maafisa wa huduma kwa wateja kama dawati namba moja ambalo ni nembo na kilelezo cha huduma bora za benki.

“Kwani sote tunatambua kuwa dawati la huduma kwa wateja ndilo limebeba sura na kilelezo cha huduma bora zinazotolewa na benki, wamekuwa wakaifanyakazi kwa bidi kwani hata pale wateja wanapokuwa na jazba, wao wamekuwa wakijitahidi kuhakikisha kuwa wanakamilisha mahitaji yao na kuwaacha wakiwa na furaha jambo ambalo ni kipaumbele cha benki,” alisema Lilian.

Wiki ya Huduma kwa Wateja ni maadhimisho ya umuhimu wa huduma kwa wateja na ya watu ambao wanahudumia na kusaidia wateja kila siku. 

Hafla hiyo huadhimishwa kila mwaka wakati wa wiki ya kwanza ya Oktoba na wafanyabiashara wote na mashirika yanayolenga huduma kote ulimwenguni, ambayo hutambua umuhimu wa kutoa huduma bora kwa wateja.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages