LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 22, 2020

MPIGIENI KURA ZA TSUNAMI DK MAGUFULI-OKASH

Mgombea Ubunge Viti Maalumu Mkoa wa Dodoma kupitia CCM, Halima Okash akielezea sera na mafanikio ya ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mgombea Urais wa CCM, Rais Dk. John Magufuli,  alipokuwa akiwaombea kura wagombea wa CCM, akiwemo  Dk. Magufuli, Mgombea Ubunge Jimbo la Chemba, Mohammed Monni na Mgombea Udiwani wa Kata ya Soya, Mashaka Mashaka.

Wananchi wakisikiliza kwa makini wakati Okash, akimwaga sera na mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano katika kuwaletea wananchi maendeleo.


Okash (wa pili kulia), akiwa na baadhi ya viongozi wa Umoja wa Wanawake (UWT).


Wananchi wakimsikiliza kwa makini Mgombea Ubunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Dodoma, Okash akifanya kampeni katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Soya.
Mgombea Udiwani Kata ya Soya kupitia CCM, Mashaka Mashaka (kushoto), akinadiwa na Okash kwa wananchi wakati wa mkutano huo wa kampeni.


Na Mwandishi Wetu, Chemba

MGOMBEA Ubunge Viti Maalumu Mkoa wa Dodoma kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Halima Okash amewaomba wananchi kumpigia kura za tsunami Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli Oktoba 28, mwaka huu, ili kumlipa wema kwa mambo makubwa aliyoifanyia Tanzania.

Okash alitoa ombi hilo kwa unyenyekevu huku akiwa amepiga magoti, alipofanya mikutano ya ndani na ya hadhara katika Kata ya Soya, wilayani Chemba, Dodoma.

"Msidanganyike kabisa na vyama vingine, kwani maendeleo yameletwa na CCM na yataendelea kutekelezwa na CCM. Tumlipe wema Dk. Magufuli aliyeifanyia mambo makubwa Tanzania kwa kumpigia kura za Tsunami Oktoba 28, 2020, kwani wema hulipwa kwa wema,"alisema Okash.

Akiwa katika kata hiyo, Okash alifanya vikao vya ndani kwa viongozi wa kata, vikao na wanawake na hatimaye kwenye mkutano hadhara ambapo alielezea mambo mazuri yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Dk. Magufuli.

Alitumia fursa ya vikao hivyo kuwaombea kura pi, Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chemba, Mohammed Monni na Mgombea Udiwani wa Kata ya Soya, Mashaka Mashaka.



No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages