LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 25, 2020

SHAMBULIZI LA ANGA LA ISRAEL LAUA SHAHIDI WAPALESTINA 4 GAZA

Shambulizi la anga la Israel laua shahidi Wapalestina 4 GazaWapalestina wanne wameuawa shahidi baada ya ndege za kivita za utawala wa Kizayuni wa Israel kushambulia kwa mabomu maeneo kadhaa ya Palestina huko mashariki mwa Ukanda wa Gaza.

Raia hao wa Palestina inayokaliwa kwa mabavu waliouawa katika hujuma hiyo ya anga ya jeshi katili la Israel jana Jumatatu wametambuliwa kama Iyad Jamal al-Jidi, Muataz Amir al-Mubid, Yahya Fareed al-Mubid na Yaaqoub Zaydieh.

      
  •  

Habari zaidi zinasema kuwa, Wapalestina hao wameuawa shahidi wakiwa katika kambi ya kijeshi ya harakati ya Jihadul Islami, katika mji wa Shejaiya, mashariki mwa Gaza.

Vijana wa Kipalestina waliouawa shahidi jana Jumatatu

Hata hivyo utawala haramu wa Israel unadai kuwa haujahusika na shambulizi hilo la anga, na eti vijana hao wa Kipalestina wameaga dunia baada ya kuripukiwa na bomu walilokuwa wakiliunda.

Eneo la Ukanda wa Gaza mbali na kushuhudia mashambulizi ya mara kwa mara ya jeshi katili la Israel, kwa zaidi ya miaka 14 sasa limekuwa chini ya mzingiro wa anga, baharini na nchi kavu unaotekelezwa na utawala ghasibu wa Israel.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages