LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 31, 2020

MADAKTARI WATATU WA KIISLAMU NI MIONGONI MWA WATU WA MWANZO WALIOFARIKI KWA CORONA NCHINI UINGEREZA

Madaktari watatu wa Kiislamu ni miongoni mwa wahanga wa mwanzo waliofariki kwa Corona nchini Uingereza
  • Viongozi wa serikali ya Uingereza wamesema kuwa, katika vifo vya mwanzo vilivyotokana na virusi vya Corona katika safu ya madaktari nchini humo, ni pamoja na madaktari watatu Waislamu.
Taarifa iliyotolewa na maafisa wa Uingereza imebainisha kuwa, madaktari hao Waislamu waliopoteza maisha katika safu ya mwanzo ya vifo vya madaktari, ni wahajiri. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mmoja wa madaktari hao watatu wa Kiislamu waliopoteza maisha kwa ugonjwa wa Covid-19 kabla ya kuenea virusi hivyo alikuwa akifanya kazi nchini Saudia na Sudan.

Boris Johnson Waziri Mkuu wa Uingereza, ambaye nchi yake haina vivaa vya tiba vya kutosha kwa ajili ya madaktari.

Imeendelea kufafanua kuwa, baada ya kuenea virusi vya Corona nchini Uingereza aliamua kurejea nchini humo ili asaidie kutoa huduma za kitaifa katika kukabiliana na maradhi hayo. Hii ni katika hali ambayo wahudumu wa afya katika hospitali za Uingereza hawana mavazi, maski wala vifaa vingine vya tiba vya kutosha kwa ajili ya kukabiliana na virusi vya Corona, na ni kwa ajili hiyo ndio maana wahudumu wengi wako hatarini kukumbwa na maradhi hayo. Hii ni katika hali ambayo wakuu wa hospitali za nchi hiyo wametahadharisha kwamba, siku chache zijazo vituo vya matibabu nchini humo vitakumbwa na Tsunami ya maambukizi zaidi ya virusi vya Corona.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages