LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 2, 2019

WASANII MAARUFU NCHINI WAJIPANGA KUTANGAZA UTALII WA NDANI.

Na Abdullatif Yunus wa Michuzi TV.

Jumla ya Wasanii wapatao Saba wanaendelea na ziara yao ya kutembelea Baadhi ya Hifadhi za Taifa hapa Nchini, lengo ikiwa ni sehemu ya kujionea Vivutio katika Hifadhi hizo ili kuendelea kuzitangaza na kuhamasisha wageni na wenyeji kufika Nchini kwetu kwa ajili ya kufanya Utalii.
Ziara hiyo iliyoanzia katika Hifadhi ya Taifa ya Burigi Chato, mara baada ya Uzinduzi wa Hifadhi za Taifa za Ibanda - Kyerwa na Rumanyika Karagwe, ikiongozwa na Waziri mwenye dhamana Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangala (MB), pamoja na wasanii wa Muziki na  Maigizo  (Bongo Movie) ambao ni Steve Nyerere, Dude, Richie, Shilole, Ebitoke,  Shetta huku kutoka Visiwa vya Zanzibar wakiwakilishwa na Msanii wa Muziki AT.
Wakiwa Katika Hifadhi ya Taifa ya Burigi Chato, wamejionea wanyama mbali mbali kama Twiga, Swala, Pundamilia, na Pofu, Wasanii hao baada ya kufanya Game Drive pamoja na matembezi ya Miguu (walking safari)wamekiri kufurahishwa na mandhali nzuri ya Hifadhi ya Burigi - Chato, kwa kujionea uzuri wa ziwa Burigi, huduma nzuri na ukarimu kutoka kwa wahifadhi, na zaidi huduma ya Malazi na mapumziko kwenye mahema mazuri ya kisasa ya Mwekezaji wa kwanza katika hifadhi hiyo aitwae Wilbard Chambulo.
Kumalizika kwa Ziara hiyo katika Hifadhi hiyo ya Burigi - Chato, na kuelekea katika Hifadhi ya Taifa ya Rubondo ambapo huko wamefanya utalii wa kwenye Maji kwa kutembelea maeneo mbalimbali, huku wajionea Viboko, Mamba,  na Ndege wazuri wa kila aina, akiwemo Ndege aina ya Conorad wenye uwezo wa Kusafiri kwa kuhama kwenda Ulaya na kurudi, lakini zaidi wakipata nafasi ya kufanya Utalii wa Uvuvi (Sport Fishing).

 Twiga hifadhini Burigi
 Msanii Steve Nyerere akionekana m wenye wasiwasi wakatiu wa game drive. Ni hadi wahifadhi walipomhakikishia kwamba wanyama hawana nongwa na binadamu ndipo akatulia...
Twiga anayepatikana ndani ya Burigi - Chato, ambae kwa mujibu wa Steve Nyerere, amedai amemsikia akiongea kingereza.... 
Pundamilia wakionekana kufurahia baada ya kuwaona (bure) wasanii ndani ya Hifadhi ya Taifa ya  Burigi - Chato. 
 Tumbili akimshangaa msanii JB
Kambi ya kitalii ya Mahema mazuri na ya kisasa ya Mwekezaji wa kwanza katika hifadhi ya Taifa ya Burigi aitwae Wilbard Chambulo.
 Ndege aina ya Conorad mwenye uwezo wa kusafiri kutoka Ulaya au kwenda kulingana na msimu wa hali ya hewa, akiwa ametulia ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Rubondo

Wasanii wakiwa wameongozana na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala katika matembezi ya Kitalii (walking) Mara baada ya kuwasili katika hifadhi ya Taifa ya Burigi Chato
 Wasanii wakiwa wameongozana na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala katika matembezi ya Kitalii (walking) Mara baada ya kuwasili katika hifadhi ya Taifa ya Burigi Chato
Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala na wasanii wakiwa katika walking safari baada ya kuwasili katika hifadhi ya Taifa ya Burigi, Chato
Mnyama aina ya Sitatunga kama alivyokutwa na Kamera yetu ndani ya hifadhi ya Taifa ya Rubondo

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages