LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 3, 2019

VIKOSI VYA HAFTAR VYAUA RAIA 14 KATIKA MJI MKUU WA LIBYA, TRIPOLI

  • Vikosi vya Haftar vyaua raia 14 katika mji mkuu wa Libya, TripoliKundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya linaloongozwa na Khalifa Haftar linatuhumiwa kufanya mashambulizi ya anga katika mji mkuu wa nchi hiyo Tripoli ambayo yameua raia 14.
Serikali ya Muafaka wa Kitaifa yenye makao makuu yake mjini Tripoli na inayoungwa mkono na jamii ya kimataifa imelaani vikali mashambulizi hayo, ingawaje haijataja idadi ya wahanga wa hujuma hiyo.
Hata hivyo vikosi waitifaki wa serikali hiyo inayoongozwa na Waziri Mkuu, Fayez al-Sarraj jana Jumatatu vilisema kuwa, mashambulizi hayo mapya ya wapiganaji wa Haftar yameua watu 14, aghalabu yao wakiwa ni wanawake na watoto wadogo.
Wanamgambo wa kamanda huyo muasi walilenga kijiji cha Al-Sawani, kusini magharibi mwa Tripoli, siku chache baada ya kushambulia kwa mabomu pia mji wa Umm al-Aranib, yapata kilomita  765 kutoka Tripoli.

Sehemu ya uharibifu unaofanywa na hujuma za anga Libya
Wakaazi wa mji wa Umm al-Aranib jana Jumatatu walifanya maandamano huku wakichoma matairi na kufunga mabarabara, kulalamikia mashambulizi hayo ya wapiganaji wa Haftar.
Tarehe 4 Aprili mwaka huu Haftar anayeungwa mkono na Saudia, Marekani na waitifaki wao wa Magharibi wa Kiarabu aliwaamuru wapiganaji wake waushambulie mji mkuu Tripoli kwa shabaha ya kuudhibiti, hatua ambayo imelaaniwa na jamii ya kimataifa. Zaidi ya watu 1,000 wameuawa na wengine wasiopungua 5,700 wamejeruhiwa katika hujuma hizo za wapiganaji wa Haftar.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages