LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 1, 2019

KITUO CHA AFYA KOME KUPEWA X-RAY YA KIDIGITALI

  Mbunge wa Buchosa Mhe.Charles Tizeba akiongea na wananchi  wa kisiwa cha Kome, wakati wa ziara ya Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu (hayupo kwenye picha) katika kisiwa hicho.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na Wananchi waliofika kwenye mkutano, wakati alipofanya ziara katika Kisiwa cha Kome Jijini Mwanza.
  Wananchi waliofika kwenye mkutano, kumsikiliza Waziri wa Afya Mhe Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara katika Kisiwa cha Kome Jijini Mwanza.
 Kitanda cha upasuaji pamoja na mashine yake kilicho katika kituo cha Afya Kome, katika Kisiwa cha Kome Jijini Mwanza,  ambacho kitawasaidia akina mama wajawazito wanapopata uzazi pingamizi.
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akiwasalimia wananchi wa kisiwa cha Kome baada ya Mkutano wa kuwasikiliza kero zao kumalizika.
 Waziri Ummy Mwalimu akimjulia hali Bi. Ester Juma, mzazi aliyejifungua katika kituo cha Afya Kome, kisiwa cha Kome kilichopo Mkoa wa Mwanza.
 Waziri Ummy Mwalimu akimjulia hali Bi Adela Deus aliyekuwa akipokea huduma baada ya kujifungua katika kituo cha Afya Kome.
 Waziri wa Afya  Mhe.@umwalimu Ummy akikabidhi moja ya vitanda kumi na moja  vya wagonjwa vilivyonunuliwa na Mbunge wa jimbo hilo Mhe. Charles Tizeba.


Na.Catherine Sungura,Buchosa

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameahidi kuwapatia mashine ya x-ray ya kisasa ya kidigitali kituo cha afya kome kilichopo halmashauri ya Buchosha wilayani Sengerema.

Waziri Ummy ametoa ahadi hiyo akiwa kwenye ziara ya kikazi kisiwani hapo ya kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

“Ninawaahidi wananchi nitaleta x-ray mashine ya kidigitali kwenye kituoa hichi cha afya ili msivuke maji kwenda kupata huduma za vipimo wilayani sengerema".Alisema Waziri Ummy

Aidha, alimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buchosha Crispian Luanda pamoja na Mganga Mkuu wake Dkt. Ernest Chacha  kwa jitihada kubwa wanazofanya za kuboresha huduma za afya kwenye halmashauri hiyo"Nimefurahi kumuona daktari wa upasuaji kwenye kituo hiki na hongereni kwa kumpatia mafunzo ya mwaka mzima kwenye eneo hili,sasa mnatakiwa kuweka vifaa na huduma za mtoto njiti ili kusiwepo na vifo vya watoto hao endapo itatokea".

Hata hivyo Waziri Ummy aliwataka akina mama wa kisiwa hicho kuhudhuria kliniki mara nne mara wanapokuwa wajawazito ili kuepukana na vifo vya wajawazito na watoto pamoja na kuepusha kuzaa watoto walemavu.

"Tumeanzisha huduma za upasuaji kwenye kitua hiki cha afya tunataka mama mjamzito wa Kome akipata tatizo la mtoto kukaa vibaya tumboni au mama akipata kifaa cha mimba asaidiwe hapa hapa"Alisisitiza Waziri Ummy.

Naye Mbunge wa Buchosa Dkt. Charles Tizeba ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Afya kuwajengea jengo la upasuaji pamoja na vifaa hivyo kuondoa tatizo kubwa la upasuaji lililokuwa linawakabili wananchi wa Kome na kuomba wizara kuwapatia vifaa vya vipimo katika vituo vya huduma za afya kwenye halmashauri hiyo kwani wananchi wameanzisha ujenzi wa zahanati 30 kwa nguvu zao hivyo wakikamilisha miundombinu huduma za afya zitakuwa zimeboreshwa kwenye jimbo lake.

Kisiwa cha Kome kimeongeza idadi ya akina mama wanaojifungulia kwenye vituo vya huduma za afya kutoka asilimia 42 mwaka 2015 kati ya akina mama 100 hadi kufikia asilimia 80 kwa mwaka  ambapo wastani wa akina mama 50 wanajifungua kwa mwezi.
-Mwisho-

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages