LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 23, 2019

WAASI 14 KUTOKA DRC WAUAWA KTIKA MAPIGANO MAGHARIBI MWA BURUNDI

Vyombo vya usalama nchini Burundi vimetangaza kuwa, bundukki zisizopungua 11 na zana zingine za kijeshi zimekamatwa katika sokomoko hilo.
Moise Nkurunziza, naibu msemaji wa jeshi la polisi nchini Burundi amesema kuwa, wabeba silaha hao wanasadikiwa kuwa wametokea katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Mapigano kati ya vikosi vya usalama na ulinzi vyya Burundi  na kundi hilo la wapiganaji yalianza mapema asubuhi ya jana Jumanne katika mkoa wa Bubanza, lakini taarifa ya mapigano hayo haikuweza kutolewa papo hapo, kulingana na kile kilichoelezwa na jeshi kwamba, lilikuwa likisubiri kulitokomeza kundi hilo.
Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi
Baadhi ya duru zinasema kuwa, wapiganaji wengi walionekana katika Wilaya za Mpanda, Gihanga na eneo la Mitakataka, mkoani Bubanza  nchini Burundi tangu mwishomi mwa wiki iliyopita wakijaribu kuingia katika msitu wa Kibira baada ya kuvuka Mto Rusizi unaotenganisha Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Burundi.
Kundi la waasi la Red-Tabara limekiri kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa wapiganaji wake ndio waliokabiliana vikali na vikosi vya usalama na ulinzi vya Burundi katika mapigano yaliyotokea jana na kwamba wanaendelea kuingia nchini Burundi kwa lengo la kurejesha utawala wa sheria. 

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages