LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 19, 2019

UKARABATI MELI YA MV VICTORIA NA MV BUTIAMA WAENDELEA KWA KASI



Ukarabati wa Meli ya Mv.Victoria na Mv Butiama katika Ziwa Victoria unaendelea kwa kufunga vifaa vipya na Vyakisasa,Ukarabati huo unatarajiwa kukamilika mwezi wa tatu mwaka 2020.
Hayo yamesemwa na makandarasi anayefanya ukarabati wa meli hizo,na kusema kuwa kwasasa wanaendelea na kazi ya kufunga genereta mpya na kupaka rangi.
  
Taarifa Zaidi.
Ukarabati unaofanywa na kampuni ya KTMI ya Korea Kusini  kwa kushirikiana  Kampuni ya Songoro Marine ya Tanzania unaendelea kwa kufunga vifaa vipya na vya kisasa ili meli hizo ziweze kutoa huduma ya usafiri katika Ziwa Victoria..

Mkurugenzi anayesimamia Miundombinu ya Uchukuzi kutoka Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Sekta ya Uchukuzi Mhandisi Thomasi Ngulika amesema kuwa ukarabati wa meli hizo umefikia asilimia Hamsini na kazi hiyo ni yamiezi kumi na Mbili..
Nae Meneja Mradi wa kampuni ya KTMI  kutoka Korea Kusini Chang Hwan  Lee amesema kuwa mradi huo utakamilika mapema mwezi wa tatu mwaka 2020.
Baadhi ya vijana wanofanyakazi katika meli hiyo akiwemo kijana Raymond Msuya ambaye anafanya kazi katika ukarabati wa meli ya Mv Victoria,wameiomba Serikali kuwapatia Ajira ya kudumu kwani wamepata elimu ya kukarabati meli kutoka kwa wakorea ambao wanafanya nao kazi.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages