Jengo la NSSF Njombe.
Majengo ya kisasa yameanza kushamiri katika Mkoa mpya wa Njombe ambao ulianzishwa rasmi mwaka 2012. zimeanza kujengwa majengo ya kisasa ya serikali, hoteli na ya watu binafsi. Pia imejengwa stendi mpya ya kisasa, soko la kisasa.
Agreement Hotel
Kanisa la Katoliki la ST Joseph la Njombe Mjini
Baadhi ya majengo yanayochepuka Njombe Mjini
Mtaa wa Mlowezi katikati ya Mji wa Njombe
Benki ya NMB Njombe
Jengo la CCM Mkoa wa Njombe lililopo Mjimwema
Soko Kuu la kisasa la ghorofa Mjini Njombe likiwa katika hatua za ujenzi
Moja ya vituo vipya vya mafuta vilivyopo Njombe. (PICHA ZOTE KAMANDA RICHARD MWAIKENDA)
Majengo ya kisasa yameanza kushamiri katika Mkoa mpya wa Njombe ambao ulianzishwa rasmi mwaka 2012. zimeanza kujengwa majengo ya kisasa ya serikali, hoteli na ya watu binafsi. Pia imejengwa stendi mpya ya kisasa, soko la kisasa.
Agreement Hotel
Kanisa la Katoliki la ST Joseph la Njombe Mjini
Baadhi ya majengo yanayochepuka Njombe Mjini
Mtaa wa Mlowezi katikati ya Mji wa Njombe
Benki ya NMB Njombe
Jengo la CCM Mkoa wa Njombe lililopo Mjimwema
Soko Kuu la kisasa la ghorofa Mjini Njombe likiwa katika hatua za ujenzi
Moja ya vituo vipya vya mafuta vilivyopo Njombe. (PICHA ZOTE KAMANDA RICHARD MWAIKENDA)
Mkoa wa Njombe ni mmojawapo kati ya mikoa mipya nchini Tanzania wenye postikodi namba 59000 [1], ukiwa umeanzishwa rasmi mwaka 2012[2]. Umepakana na mikoa ya Morogoro, Ruvuma, Mbeya na Iringa.
Kutokana na hadhi mpya, wilaya ya Njombe imegawanyika kati ya ile ya mjini na ile ya vijijini. Pia, mwezi wa Machi 2012, imeanzishwa wilaya ya Wanging'ombe.
Mwaka 2012 katika eneo hilo kulikuwa na wakazi 702,097 Census 2012. Jalada kutoka ya awali juu ya March 5, 2016. Iliwekwa mnamo 14 February 2016. katika wilaya sita zifuatazo: Njombe Mjini (wakazi 130,233), Njombe Vijijini (wakazi 85,747), Makambako (wakazi 93,827), Makete (wakazi 97,266), Ludewa (wakazi 133,218), Wanging'ombe (wakazi 161,816).
Makao makuu yako Njombe mjini.
Kabila la Wabena liko wilaya ya Njombe na eneo la Malangali likiwa linapakana na wilaya ya Ulanga na wilaya ya Kilombero (Mkoa wa Morogoro), Wakinga wako wilaya ya Makete na Wapangwa wako katika wilaya ya Ludewa.
Yapo pia makabila madogo kama vile Wawanji, Wakisi, Wamanda, Wamagoma n.k. ambao kwa ujumla wao wanachukua asilimia 6 iliyosalia ya watu Mkoani Njombe.
Karibu wakazi wote wa mkoa ni Wakristo, hasa Walutheri na Wakatoliki.
Majimbo ya bunge[hariri | hariri chanzo]
Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:
- Njombe Kaskazini : mbunge ni Joram Hongoli (CCM)
- Njombe Kusini : mbunge ni Edward Mwalongo (CCM)
- Makambako : mbunge ni Deo Kasenyenda Sanga (CCM)
- Wanging'ombe : mbunge ni Gerson Hosea Lwenge (CCM)
- Makete : mbunge ni Dk. Norman Adamson Sigalla (CCM)
- Ludewa : mbunge ni Deo Ngalawa.
- Mkoa huo hivi sasa unaongozwa na Mkuu wa Mkoa, Christopher Ole Sendeka.
No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇