Na Lydia Lugakila Bukoba
Jumla ya Wakulima wapatao 5,000 wanatarajia kufikiwa na mradi wa kilimo bora cha migomba katika kata zilizopo kando kando ya ziwa ikimba katika Halmashauri ya Bukoba mkoani Kagera.
Hayo yamebainishwa leo oktoba 22, 2019 na Afisa Ugani Deusdedit Rweyemamu anayesimamia eneo laziwa ikimba wakati alipotembelewa na wana mradi ambapo amesema mradi huo ulianza februari mwaka huu na kwamba lengo kubwa la mradi huo kuongeza ubora katika zao la migomba na kuwa Jumla ya Wakulima wapatao 5,000 wanatarajia kufikiwa na mradi wa kilimo bora cha migomba.
Rweyemamu amezitaja kata zenye mradi huo kuwa ni kata ya Izimbya , Rubale, Kaibanja, Kyamulaile, Ruhunga, Kikomero na Buterankuzi zilizopo mkoani hapa.
Aidha ameongeza kuwa katika kata ya Buterankuzi kuna mashamba darasa 27, ambayo husaidia wakulima kwenda kujifunza kilimo bora cha migomba na kisha kwenda kuboresha mashamba yao.
Baadhi ya wakulima ambao wako katika mradi huo wamesema kabla ya mradi huo migomba yao ilikuwa inastawisha chane mbili za ndizi lakini kwa sasa kutokana na elimu waliyoipata tayari wameanza kustawisha migomba mizuri ambapo wanatarajia itakuwa na chane kuazia kumi na kuendelea
Hayo yamebainishwa leo oktoba 22, 2019 na Afisa Ugani Deusdedit Rweyemamu anayesimamia eneo laziwa ikimba wakati alipotembelewa na wana mradi ambapo amesema mradi huo ulianza februari mwaka huu na kwamba lengo kubwa la mradi huo kuongeza ubora katika zao la migomba na kuwa Jumla ya Wakulima wapatao 5,000 wanatarajia kufikiwa na mradi wa kilimo bora cha migomba.
Rweyemamu amezitaja kata zenye mradi huo kuwa ni kata ya Izimbya , Rubale, Kaibanja, Kyamulaile, Ruhunga, Kikomero na Buterankuzi zilizopo mkoani hapa.
Aidha ameongeza kuwa katika kata ya Buterankuzi kuna mashamba darasa 27, ambayo husaidia wakulima kwenda kujifunza kilimo bora cha migomba na kisha kwenda kuboresha mashamba yao.
Baadhi ya wakulima ambao wako katika mradi huo wamesema kabla ya mradi huo migomba yao ilikuwa inastawisha chane mbili za ndizi lakini kwa sasa kutokana na elimu waliyoipata tayari wameanza kustawisha migomba mizuri ambapo wanatarajia itakuwa na chane kuazia kumi na kuendelea
No comments:
Post a Comment
ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇