LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 15, 2019

MIKOA YA KANDA YA ZIWA YAONGOZA MATOKEO DARASA LA SABA


Katibu Mkuu wa baraza la mitihani la Taifa, Dkt. Dkt Charles Msonde.

Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
MIKOA ya kanda ya ziwa yaongoza matokeo ya kumaliza elimu ya Msingi kwa kuongoza kwa shule 10 bora zote zikitokea katika mikoa ya Mara, Kagera na shinyanga. 

Shule kumi zilizofanya vizuri katika matokeo ya kumaliza elimu ya msingi hapa nchini ni, Graiyaki ya Mkoa wa Mara, Twibhoki Mara, Kemebos ya Kagera , Little Treasures Mkoa wa Shinyanga na Mkoa wa Mwanza shule ya Musabe. 

Hata hivyo shule nyingine ni Tulele ya mkoani Mwanza, Kwema Modern ya Mkoa wa shinyanga pia, Peaceland, Mugini ya Mwanza na Rocken Hill mkoa wa Shinyanga. 

Akitangaza matokeo ya Darasa la Saba leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa baraza la mitihani la taifa (NECTA) , Dkt Charles Msonde amesema kuwa katika matokeo ya waliofanya mtihani ni  asilimia 81.5 sawa na watahiniwa 933,369 waliofanya mtihani huo wamefaulu.

Dkt. Msonde amesema kuwa kwa mwaka huu 2019 ufaulu umeongezeka kwa asilimia 3.78 wakati shule za mikoa ya kanda ya ziwa ikiwa kinara kwa kuongoza.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages