LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 21, 2019

HUDUMA YA MAJI KEREGE HADI AMANI BAGAMOYO KUREJEA LEO USIKU



MAMLAKA ya majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imewahakikishia wananchi waishio maeneo ya Kerege hadi Amani, Bagamoyo kuwa jitihada za kurejesha huduma za maji zipo katika hatua za mwisho kabisa ambapo usiku wa leo kazi hiyo inatarajia kumalizika.


Kupitia taarifa iliyotolewa na Mamlaka hiyo iliyotolewa leo Oktoba 21, imeeleza kuwa kasi ya urekebishaji wa bomba hili imechukua muda kuliko ilivyotarajiwa kufuatia kuendelea kuwepo kwa maji mengi katika mto Mpiji.

Imeelezwa kuwa  maeneo ya Kerege, Mapinga, Kiharaka, Kiembeni, Mingoi, Kimelela, Vikawe na Amani yamekosa maji tangu Oktoba 19 siku ya Jumamosi kufuatia kukatika kwa bomba kuu la inchi 54 linalosafirisha maji kutoka mtambo wa Ruvu chini hali iliyosababishwa na uchimbaji holela wa mchanga katika mto Mpiji.

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages