LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Apr 19, 2019

MAHAKAMA YA JUU UGANDA: MUSEVENI ANAWEZA KUGOMBEA URAIS 2021

Wakiongozwa na Jaji Mkuu Bart Katureebe, Majaji wanne walitupilia mbali kesi hiyo ya upinzani huku Majaji watatu wakisema bunge halikufuata sheria wakati wa mabadiliko hayo. Uamuzi huo sasa unampa nafasi Rais Museveni ambaye amekuwa akiongoza Uganda tangu mwaka 1986 ya kuwania tena kiti hicho mwaka 2021 na kuendelea hadi mwaka 2026.
Mwanasheria Mkuu wa serikali Mwesigwa Rukutana amesema uamuzi huo wa Mahakama ni ushindi kwa wananchi wa Uganda.
Hata hivyo, wakili wa upinzani Erias Lukwago, amesema demokrasia ipo katika hali ngumu. Ameongeza kuwa, n masikitiko makubwa, lakini barani Afrika, ni miujiza kushinda kesi dhidi ya serikali iliyo madarakani.
Kizza Besigye, kiongozi mkongwe wa upinzani nchini Uganda
Upinzani dhidi ya mabadiliko hayo ya sheria ulimuibua Mbunge kiijana Robert Kyagulanyi al-maaruufu Bobi Wine, ambaye kwa sasa  amekuwa kama kinara wa upinzani na mwiba mkali dhidi ya serikali ya Museveni ndani na nje ya bunge la nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
Wapinzani nchini Uganda wanalalamika na kuituhumu serikali ya Rais Yoweri Kaguta Museveni kwamba, imekuwa ikiendesha siasa za mkono wa chuma dhidi ya mrengo wa upinzani, hatua ambayo wanaitaja kuwa, inakandamiza na kubinya demokrasia katika nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages