LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 30, 2019

WAZIRI ANGELA KAIRUKI APOKEWA OFISINI JIJINI DODOMA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama akisalimiana na Waziri wa Nchi Ofisi hiyo anayeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki wakati alipokutana na watumishi wa Ofisi yake Januari 30, 2019 Jijini Dodoma
 NA MWANDISHI WETU
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki amekutana na watumishi wa ofisi yake kwa mara ya kwanza tangu alipoteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli kushika wadhifa huo mpya.
Waziri Kairuki amekutana na watumishi hao mapema hii leo (Januari 30, 2019) katika Ofisi hiyo Jijini Dodoma na kuzungumza nao ikiwa ni sehemu ya kufahamiana na kujua ofisi hiyo.
Mkutano huo uliohudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama pamoja na Naibu wake Mhe.Anthony Mavunde pamoja na Makatibu wakuu wa Ofisi hiyo Bi.Maimuna Tarishi anayeshughulikia Bunge na Waziri Mkuu pamoja na Dorothy Mwaluko anayeshughulikia Sera, Uratibu na Uwekezaji.
Kairuki waliwataka watumishi hao kuendelea kufanya kazi kwa umoja na uzalendo ili kujilete maendeleo nchini na kuahidi kushirikiano nao kwa kipindi chote atakachokuwa katika Ofisi hiyo.
“Kipekee ninawashukuru viongozi na watumishi wote wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mapokezi mazuri na  hii ni ishara ya umoja wenu na ninaahidi kushirikiana na watendaji wote katika utekelezaji wa majukumu tuliyonayo  kwa maslahii mapana ya ofisi yetu na Taifa kwa ujumla,”alisisitiza Kairuki
Naye Waziri wa Nchi wa ofisi hiyo Mhe.Jenista Mhagama alipongeza watumishi wa Ofisi yake kwa kuendelea kutekeleza majukumu na kuwataka kuwa na uzalendo na weledi wa hali ya juu.
“Ninachoweza kusema tutaendelea kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa kazi za kila siku kwa kuzingatia kuwa hii ni familia moja yenye nia moja ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Mhe.Rais ili kujiletea maendeleo katika nchi yetu,”alisema Mhagama.
 Waziri wa Nchi Ofisi hiyo anayeshughulikia Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki akisalimiana na  Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde wakati wa mkutano huo na watumishi wa ofisi yake Januari 30, 2019.
 Waziri wa Nchi Ofisi hiyo anayeshughulikia Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki akisalimiana na Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bi. Dorothy Mwaluko.
 Waziri wa Nchi Ofisi hiyo anayeshughulikia Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Ofisi hiyo alipokutana nao Januari 30, 2019 katika Ofisi hiyo Jijini Dodoma.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama akizungumza na watumishi wa ofisi yake walipokutana nao mapema hii leo
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki akizungumza na watendaji wa Ofisi yake (hawapo pichani) walipokutana kuzungumza nao Jijini Dodoma, kulia ni Waziri wa Nchi ofisi hiyo, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama na wa kwanza kushoto ni Naibu wake Mhe. Anthony Mavunde.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mhe.Angellah Kairuki pamoja na Mhe.Jenista Mhagama pamoja na Naibu wake Mhe.Anthony Mavunde wakiwa katika ofisi hiyo walipokutana na Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu hii leo.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi.Maimuna Tarishi akizungumza jambo wakati wa mkutano wao na Mawaziri wa Nchi wa Ofisi hiyo walipokutana Januari 30, 2019 Jijini Dodoma.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mhe.Angellah Kairuki akizungumza jambo na Viongozi wa Ofisi hiyo alipokutana nao ofisini kwake hii leo, wa kwanza kushoto ni Waziri wa Nchi ofisi hiyo anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama pamoja na Naibu wake Mhe.Anthony Mavunde.
 Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakisubiri kuzungumza na Waziri wa Nchi Ofisi hiyo anayeshughulikia Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki alipokutana nao kujadili masula ya ofisi yao Januari 30, 2019. (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages