LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 17, 2018

MOI YASAINI MKATABA NA HOSPITALI YA KIMATAIFA CHINA


Dar es Salaam, 17/08/2018. Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) imesaini mkataba wa ushirikiano na hospitali ya kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha Beijing nchini China. Mkataba huo utajikita katika maeneo ya tiba, utafifi na mafunzo.

Mkataba huo umesainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface pamoja na Rais wa hospitali ya kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking Ms Hongxia Yu ambapo MOI itanufaika katika kuboresha huduma za kibingwa za daraja la juu (Super specialised services) katika maeneo ya upasuaji wa Mifupa, Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu.

Hafla ya kusaini mkataba huo imeshuhudiwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh Ummy Mwalimu pamoja na Balozi wa Tanzania nchini China Mh. Balozi Mbelwa Kairuki pamoja na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhamad Kambi.

Aidha, hatua hiyo imefikiwa baada ya Waziri wa Afya Mh Ummy Mwalimu ambaye yuko kwenye ziara ya kikazi nchini China kufanya kikao na Rais wa Hospitali ya kimataifa ya chuo kikuu cha Peking jijini Beijing kuhusiana na kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuboresha huduma za tiba za kibingwa hapa nchini.

Hospitali ya kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking ina uzoefu mkubwa katika matibabu ya Mifupa, Ubongo, Mgongo na Mishipa ya fahamu ambapo ina vitanda 1800 vya kulaza wagonjwa, ICU vitanda 171, Vyumba vya upasuaji 48 na kwa mwaka inahudumia zaidi ya wagonjwa milioni 14.7



No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages