LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 16, 2018

WIZARA YA MADINI YAMTAKA MSHAURI ELELEKEZI MRADI WA SMMRP KUTOMUHOFIA MKANDARASI

 Wizara ya Madini imekabidhi eneo la ujenzi wa Kituo cha Umahiri wilayani Songea Mkoani Ruvuma ikiwa ni utekelezaji  wa Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini   (SMMRP)   wa   Ujenzi   wa   Kituo   cha   Umahiri   wenye   lengo   la   kusaidia kuwaongezea ujuzi wachimbaji wadogo kwa kutiliana saini za ujenzi na Mkandarasi wa vituo hivyo kampuni ya SUMA JKT na kampuni ya Y&P akiongea   wakati   wa   Makabidhiano   hayo   kwa   niaba   ya   Katibu   Mkuu   Wizara   ya Madini,   Mkurugenzi  wa   Sheria   Kutoka   Wizara   hiyo   Bw.   Edwin   Igenge   amemtaka Mshauri elekezi wa Mradi huo kampuni ya Y&P kumsimamia mkandarasi ambayo nikampuni   ya   SUMA   JKT   bila   hofu   ili   kuhakikisha   wanafanya   kazi   katika   viwango vilivyokubaliwa na ambavyo vipo kwenye mkataba.“Tunawakabidhi   mkataba   huu   muanze   kufanya   kazi   kama   ilivyokubaliwa,   nanakuagiza   mshauri   elekezi   uhakikishe   unamsimamia   mkandarasi   bila   woga,dhumuni   ni   kuhakikisha   anafanya   kazi   yenye   ubora   kulingana   na   mikatabatuliyoisaini leo”. Alisema Bw. IgengeAkiongea   wakati   akimkabidhi   mchoro   wa   mradi   huo,   Msanifu   Majengo   kutokaKampuni ya Y&P Bw. Benjamin Kasiga amemtaka mkandarasi kufanya kazi kamaalivyoelekezwa katika mkataba na kwa kuzingatia viwango vinavyojitajika nchini.Naye  Muwakilishi kutoka kampuni ya SUMA JKT Mhandisi Joseph Jeremiah amehidikutekeleza kulingana na maelekezo yaliyoainishwa kwenye michoro na kufanya kazikwa ubora wa hali ya juu.Hatua   hii   ni   utekelezaji   wa   ahadi   iliyotolewa  bungeni   na   Waziri   wa   Madini   Mhe.Angelah Kairuki   wakati akiwasilisha Bungeni Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2018/19 ambapo alieleza kuwa mradi huu utatekelezwa katika maeneo ya Mpanda, Songea, Chunya, Tanga, bariadi, Bukoba na Musoma pamoja na upanuzi wa miundombinu ya Chuo Cha Madini Dodoma kwaajili ya kuwezesha  utekelezaji wa shughuli za   madini zinazotekelezwa na ChamaCha Wachimbaji Madini Wanawake




No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages