LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 23, 2018

KUNDI LA AL SHABAB LASHAMBULIA KAMBI YA JESHI NA KUUWA WANAJESHI 27 SOMALIA

Kundi la wanamgambo wa al Shabab lenye makao yake nchini Somalia limetangaza hii leo kuwa limeshambulia kambi moja ya jeshi kwa kulipua bomu lililotegwa garini huko kusini mwa nchi hiyo na kuuwa wanajeshi 27.
Shambulio la leo la kundi la al Shabab dhidi ya kambi ya jeshi nchini Somalia limefanyika baada ya lile la mwezi Juni mwaka huu ambapo kundi hilo pia lilishambulia kambi nyingine ya jeshi na kujeruhiwa wanajeshi saba wa Somalia. Al Shabab inadai kuwa inapambana kwa lengo la kuiondoa madarakani serikali kuu ya Somalia na kuanzisha serikali yake itakayoendesha shughuli zake kwa mujibu wa sheria za Kiislamu.
Maafisa wa serikali ya Somalia hadi sasa hawajatoa maelezo yoyote kuhusu shambulio hilo la leo katika kambi ya jeshi huko Baar Sanguni umbali wa kilomita 50 kutoka mji wa bandari wa Kismayu. Abdiasis Abu Musab msemaji wa kundi la al Shabab anayehusika na oparesheni za kijeshi amesema kuwa kwanza kabisa walishambulia kambi ya jeshi ya askari wa serikali kwa kulipua bomu la kutegwa garini na kisha waliingia kambini humo na kuuwa wanajeshi 27 na kuidhibiti kambi hiyo.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages