Shule ya Sekondari Kom iliyopo mjini Shinyanga leo Jumamosi Novemba 11,2017 imefanya mahafali ya tisa ya kidato cha nne tangu kuanzishwa kwa shule hiyo mwaka 2006.
Wahitimu wa kidato cha nne mwaka 2017 katika shule ya sekondari Kom wakimpokea mgeni rasmi katika mahafali ya tisa ya shule hiyo,mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkurugenzi wa shule ya sekondari Kom,Jackton Koyi akimpokea mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro kwa ajili ya kushiriki mahafali ya kidato cha nne katika shule hiyo
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwapungia mkono wahitimu wa kidato cha nne shule ya sekondari Kom
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya mkurugenzi wa shule ya sekondari Kom
Mwanafunzi wa kidato cha tatu Zena Ali akimweleza Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro historia ya shule ya sekondari Kom wakati wa maonesho ya shughuli mbalimbali zinazofanyika katika shule hiyo
Wanafunzi wa shule ya sekondari Kom wakionesha ramani ya dunia kwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro wakati wa maonesho ya taaluma wakati wa mahafali hayo
Mwanafunzi wa kidato cha tatu Rajuu Masudi ambaye ni mtaalamu wa kuchora akieleza kuhusu sanaa ya uchoraji inayofanywa na wanafunzi wa shule ya sekondari Kom
Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Kom,Safia Ali akitoa maelezo kuhusu maonesho ya sayansi kwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro
Wahitimu wa kidato cha nne 2017 katika shule ya sekondari Kom wakiandamana
Wahitimu wakiandamana kuelekea ukumbini
Mgeni rasmi,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akikata utepe wakati wa mahafali ya tisa ya kidato cha nne katika shule ya sekondari Kom.Kulia ni mwenyekiti wa bodi ya shule Peter Kugulu,kushoto ni mkurugenzi wa shule ya Sekondari Kom,Jackton Koyi
Wahitimu wakiingia ukumbini
Mkuu wa shule ya sekondari Kom,Mwita Waryoba akielezea historia ya shule hiyo
Mkurugenzi wa shule ya Sekondari Kom,Jackton Koyi akizungumza wakati wa mahafali ya tisa ya kidato cha nne katika shule ya sekondari Kom
Wahitimu wa kidato cha nne wakipunga mkono
Wahitimu wa kidato cha nne,Scholastica Simon na Dickson Nyansika wakikata keki wakati wa mahafali ya kidato cha nne mwaka 2017
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akimlisha keki mhitimu wa kidato cha nne Dickson Nyansika
Mahafali yanaendelea
Wanafunzi wakiwa wamevaa mavazi mbalimbali ya ubunifu
Wanafunzi wakiimba shairi
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza
No comments:
Post a Comment
ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇