
Mwanza:
Meneja Mahusiano wa Biashara kwa Serikali wa Benki ya NMB, Humphrey
Kaaya (kushoto), akitoa maelezo kwa wakazi wa Mkoa wa Mwanza kuhusu
fursa za upatikanaji wa mikopo ya matrekta na suluhisho za kifedha
zinazowezesha ununuzi wa zana za kisasa za kilimo, wakati wa Maonesho ya
Nane Nane yanayofanyika katika Viwanja vya Nyamhongolo, mkoani Mwanza.
NMB
ni mdhamini wa Maonesho ya Nane Nane 2026, ikiwa sehemu ya dhamira yake
ya kusogeza huduma za kifedha karibu na wananchi na kuwawezesha
wakulima, wafugaji, wavuvi na wajasiriamali kuongeza tija na kukuza
uchumi kupitia huduma zinazokidhi mahitaji yao.
No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇