Benki ya NMB imewahakikishia wafanyabiashara kuendelea kuwapatia masuluhisho ya kifedha yanayolenga mahitaji ya sekta mbalimbali za uchumi. Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki katika Jukwaa la NMB Business Executive Network 2026 lililowakutanisha zaidi ya wafanyabiashara 300 kutoka Dar es Salaam na Pwani.
Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, alisema benki hiyo imeanzisha Madawati ya Kisekta ili kutoa huduma zinazolingana na mahitaji ya sekta kama madini, ujenzi, utalii, kilimo, afya na elimu. Alisema masuluhisho hayo yanajumuisha Asset Financing, Bid Bond, Advance Payment Guarantee na Performance Guarantee.
Katika jukwaa hilo, NMB pia ilitambulisha tuzo mbili za kimataifa ilizotunukiwa mwaka huu ambazo ni Tuzo ya Benki Bora zaidi kwa Wafanyabiashara Tanzania 2026 kutoka jarida la Euromoney na Tuzo ya Benki Bora zaidi kwa Wafanyabiashara Tanzania 2026 kutoka jarida la Global Finance, zikidhihirisha kutambuliwa kwake kimataifa kwa ubora wa huduma.
Jukwaa hilo lilitoa nafasi kwa wafanyabiashara na viongozi wa NMB kujadiliana kuhusu mahitaji ya sekta binafsi na namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano unaochochea ukuaji wa biashara na uchumi wa Tanzania.

No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇