Mbunge wa Viti Maalumu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Dodoma, Dkt. Neema Majule (katikati) ametoa msaada wa vyakula, vinywaji, vifaa vya usafi na vyandarua 100 kwa Shule ya Viziwi Dodoma, katika tukio lililofanyika Februari 21, 2026 katika shule hiyo iliyopo Kisasa jijini Dodoma.
Katika tukio hilo, Dkt. Majule ambaye yupo mstari wa mbele kujitotea kwa hali na mali katika masuala ya kijamii na hasa kwa watu wenye uhitaji maalumu, alitoa mchele, unga, mafuta, sukari, vinywaji, sabuni, fagio, kalamu, madaftari na pedi kwa ajili ya mabinti. Kabla ya makabidhiano ya msaada huo, Dkt. Majule alipata wasaa wa kutembelea na kujionea jinsi wanafunzi wanavyopata mafunzo kwa njia ya vitendo ikiwemo ushonaji, kompyuta, ufundi umeme na uselemala lakini pia mchezo wa pooltable. Mkuu wa shule hiyo, Awadhi Mbogo alitoa shukrani kwa kitendo cha mbunge huyo kuamua kutoa msaada huo mkubwa kwa shule hiyo na kwa aendelee na moyo huo wa kujitolea na kutoa wito kwa wananchi wengine kuiga mfano huo. Akizungumza katika tukio hilo, Dkt. Majule amesema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan akilihutumia Bunge Novemba 14, 2025, alisema anatamani kuona Tabasamu la watu wa Chini kabisa, hivyo inatakiwa "tumuunge mkono kwa kutoa misaada kwa watu hao na hasa wenye uhitaji maalumu." Aidha, Dkt. Majule amesema kuwa baada ya kufanikiwa kupata ubunge sadaka yake ya kwanza ameamua kuipeleka katika shule hiyo ya viziwi Dodoma. Shule hiyo ambayo ni ya serikali, chini ya Manispaa ya Dodoma inasimamiwa pia kwa msaada wa Robin Donker Sgoed ambaye ni Mwasisi na Mkurugenzi wa Taasisi ya Environmental Oriented and Training Support (EOTAS). Your Ad Spot
Feb 22, 2026
Home
featured
Habari
RAIS SAMIA ANATAMANI KUONA TABASAMU LA WATU WA CHINI, TWENDE TUKAGUSE MAISHA YAO- DKT. MAJULE
RAIS SAMIA ANATAMANI KUONA TABASAMU LA WATU WA CHINI, TWENDE TUKAGUSE MAISHA YAO- DKT. MAJULE
Tags
featured#
Habari#
Share This
About CCM Blog INVITEE
Habari
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot







No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇