1. Kadri unavyozidi kuwa mkimya ndivyo maneno yako yatakavyozidi kuchukuliwa kwa ukubwa na watu.
2. Usichukulie kila kitu personal kwasababu sio kila mtu anakufikiria kama ambavyo wewe unavyojifikira.
3. Ukifocus zaidi kwenye matatizo na changamoto utakuwa na matatizo mengi zaid, ukifocus kwenye kuwezekana kwa mambo utafanikisha mambo mengi.
4. Haijalishi leo inauma au unapitia maumivu kiasi gani kuna siku utatizama nyuma na kugundua ulipambana sana kuyabadilisha maisha yako ili uwe mtu bora kama ulivyo.
5. Tunakutana na watu kwa sababu, ni either ubadilishe maisha yao au wabadilishe maisha yako.
6. Usiogope kujaribu kitu/vitu vipya, maisha yanaboa sana kukaa ndani ya mipaka ya vitu ambavyo tayari unavijua na kuvizoea.
7. Hautokuja kujua umuhimu ya matukio mbalimbali katika maisha yako kaka hadi pale yatakapogeuka kuwa kumbukumbu
8. Utakapoanza kuhesabu matendo na vitu mbalimbali unayojivunia kwenye maisha yako utaanza kuwa kipofu wa vitu ambavyo hauna kwenye maisha yako.
9. Ukishindwa kucontrol mdomo na matamshi yako basi hutoweza kucontrol future yako.
10. Maisha ni kama kioo; unachokiwaza, kukihisi, kukitamka na kukipitia ni reflection nzima ya wewe ulivyo. Ukiona vitu haviko vile unavyotaka viwe jaribu kubadilika au kutafuta mabadiliko ndani yako.
11. Mtu pekee unayetakiwa kumtizama na kupambana naye kila asubuhi ni wewe mwenyewe, usishindwe..pambana.
UMEIPENDA NAMBA NGAPI?

No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇