LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 22, 2025

MWANAMKE KUWA MZURI SANA SI KIGEZO :

Mwanamke Kuwa mzuri ni Hali  ya mwonekano Katika kijamii ya kuthamini uwepo wa mwanamke aliyejitunza vizuri, ni sawa na maua Katika bustani hivyo  inapaswa kuwa ya furaha ya kawaida ambayo mwanamume humpa heshima mwanamke Kwa kujitunza.

Mwanamke mrembo ufanya mazingira mazuri ya kupumzika, kupendezwa na kushirikishwa, na haipaswi kuwa zaidi ya lugha ya kupongezwa Kwa uzuri.

‎Hakuna ubaya wowote kwa kumsifia Kwa uzuri, uzuri unaendana  na tabia. Inaweza kutumika lugha kumsifia Kwa mwonekano wa nje, inaweza kutumika kumsifia Kwa tabia, na inaweza kutumika kumsifia heshima aliyo nayo.

Lakini baadhi ya wanaume wanaona kumsifia  Mwanamke kama njia ya kufikia lengo la kumpata Mwanamke. baadhi Wanaelekea kuona kila mwanamke mrembo kama swala  wa mbugani.

‎Lakini lugha hii ya kusifia ambayo inapaswa kuwa njia  shirikishi kwa kijamii inakuwa kitu kingine katika baadhi ya matukio ambapo inageuka kuwa kusifia kwa uchafu, na ishara ya tamaa.

‎Wakati mwingine kusifia ni  hunyenyekeza na kumfanya Mwanamke aone aibu na kushindwa kutembea Kwa kujiamini. Baadhi Wanaume wanapiga  makofi au kuimba wimbo wa kumfuata Mwanamke Kwa kumsifia Kuwa mzuri.
 ‎
‎Hakuna ubaya wowote kuvutiwa na kuthamini mwonekano mzuri na wa kifahari wa Mwanamke. 

Tabia  ya kumsifia Mwanamke kama mzuri hii inakuwa ishara ya nia ya kisanii kwa baadhi ya wanaume ambao malezi yao ya kimaadili si kitu cha kawaida.

‎Katika baadhi ya matukio, mwanamume anapomsifia  mwanamke kama "wewe ni mrembo", inamaanisha tu, "Nataka kulala nawe". Kumbe sio Hivyo 

Na baadhi ya wanawake kwa sababu ya mawazo machafu yaliyopotoka wanaweza kutafsiri ishara hiyo kwa urahisi kumaanisha, "Mwanaume anataka kulala nayei". 

Baadhi ya Wanawake akisifiwa na Mwanaume Kuwa ni mzuri,  anachowaza ni ngono kumbe sio Hivyo 

‎Tumefika kwenye njia panda ambapo baadhi ya watu wanafikiri kwamba mwanamume hawezi kumkamilisha mwanamke mrembo bila Kuwa na pesa. Ni bahati mbaya sana: "Mawasiliano mabaya huharibu tabia njema"..

‎"Kujihusisha na ushawishi mbaya, makundi mabaya, au usemi mbaya (umbea, uongo, mafundisho ya uongo) kunaharibu tabia ya Mwanamke,  tabia mbaya ukufanya Mwanamke akose adabu, usiheshimike, na kutengwa na jamii  mbali na maisha ya kawaida" 

‎Baadhi ya watu wanaishi maisha ya "takataka ndani, takataka nje". Kwao, chochote kinaenda.  Wana mwelekeo wa kufikiri kwamba wanawake wameumbwa kwa ajili ya starehe ya wanaume.

‎Lakini je, mwanaume anapaswa kulala na mwanamke yeyote ambaye uzuri wake unamvutia? Je, mwanamke anapaswa kukubali kila tendo la ndoa la mwanaume aliyemsifia kwamba ni mzuri?.  ikiwa NDIO Hilo litamfanya mtu awe kama mnyama.

‎Mungu hakuwaumba wanaume wawe Casanova. Mwanaume yeyote anayeishi kwa ajili ya starehe tu, akifurahia mwili wa Mwanamke, ni sawa na mbuzi dume.

 

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages