LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 4, 2025

MAMA LISHE WAMLAKI RAIS SAMIA, WATOA YA MOYONI


Mama Lishe wamejitokeza kwa wingi kumlaki Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Samia Suluhu Hassan alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Dodoma leo Februari 4, 2025, tayari kuongoza maadhimisho ya miaka 48 ya CCM kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma kesho. CCM Itatumia maadhimisho hayo kuwatambulisha kwa wana CCM wagombea wao urais kupitia chama hicho katika uchaguzi Mkuu ujao. Samia atagombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mgombea Mwenza atakuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dkt. Emmanuel Nchimbi. Dkt. Hussein Ali Mwinyi atagombea urais wa Zanzibar.





 


IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA

MHARIRI

BLOG YA TAIFA YA CCM

0754264203


No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages