Mkuu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo ya Vijijini, Prof. Hozen Mayaya ameipongeza jamii inayoizunguka shule ya Sekondari Mbabala wilayani Dodoma, kwa kuwa na mwamko wa kupeleka watoto wao wengi wa kike katika shule hiyo.
Pongezi hizo zilitolewa kwa niaba yake na mgeni rasmi, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko wa chuo hicho, Godrick Ngoli wakati wa Mahafali ya shule hiyo yaliyofanyika shuleni hapo mwishoni mwa wiki.
Mmoja wa wanafunzi wa kike wa shule hiyo akikabidhiwa cheti na Mgeni Rasmi, Ngoli ikiwa ni ishara ya kumaliza kidato cha nne.
Baadhi ya wanafunzi wa kike waliohitimu Kidato cha Nne katika shule hiyo.
Baadhi ya wazazi na wageni waalikwa wakiwa katika mahafali hayo.
Mkuu wa shule hiyo, Patrick Mayengo akipongezwa na Mgeni rasmi, Ngoli kwa ufaulu mzuri wa shule hiyo.
Mmoja wa walimu wa shule hiyo akipatiwa zawadi.
Baadhi ya wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne wakikabidhiwa vyeti.
Mgeni rasmi Ngoli akiwa na baadhi ya viongozi akitokea kukagua jengo la maabara. Kulia ni Mkuu wa shule hiyo, Patrick Mayengo na Diwani wa Kata ya Mbabala, Paskazia Mayala.
Ngoli akikagua ujenzi wa matundu ya vyoo.
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDAMHARIRI
BLOG YA TAIFA YA CCM
0754264203
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇