Na Bashir Nkoromo, CCM Blog
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana amejiuzulu Umakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, na Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ameridhia.
"Ni kweli nilipokuomba utusaidia kwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti nilikuahidi utakaa muda mfupi kama ulivyoomba, na kwa kweli nilipenda uendelee kutusaidia lakini kwa kuwa umeomba sana na ahadi ni deni nalazimika kwa moyo mzito kuridhia kujiuzulu kwako", imesema taarifa ya Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Amos Makalla ikikariri sehemu ya majibu ya Dk. Samia kufuatia ombi la Kinana.
"Pia Mwenyekiti wa CCM amesisitiza kuwa Chama kitaendelea kutumia uzoefu na maarifa ya Ndugu Kinana kila vitakapohitajika,
Chama Cha Mapinduzi kinamshukuru Ndugu Kinana kwa mchango wake mkubwa kwa Chama chetu", amesma Makalla katika taarifa hiyo.
Your Ad Spot
Jul 29, 2024
KINANA AG'ATUKA UONGOZI CCM, DK. SAMIA ARIDHIA KWA MOYO MZITO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot


No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇