LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 7, 2024

BIL 4.8 KUTEKELEZA MIRADI YA MAJI KILOMBERO 2024-2025

 NA VICTOR MAKINDA: IFAKARA, KILOMBERO.

Meneja wa RUWASA wilaya ya Kilombero, Florence Mlelwa.

Katika kuhakikisha kuwa lengo la serikali ya awamu ya sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuwafikishia  maji safi na salama asilimia 85 ya wananchi waishio vijijiji na 95 waishio mijini mpaka kufikia mwaka 2025 linatimia,  Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro,  umepanga kutumia jumla ya
Shilingi 4,854,177,086.35 kutekeleza  miradi ya maji katika mwaka mpya wa fedha unaotarajiwa kuanza Julai Mosi 2024-2025.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ifakara mji, Kassim Nakapala, akichangia katika kikao cha wadau wa maji.

Hayo yamebainishwa leo mjini Ifakara, Wilayani Kilombero na Meneja wa wa RUWASA, wilaya ya Kilombero, Mhandisi Florence Mlelwa, wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji kwenye mkutano wa wadau wa maji uliolenga  kujadili changamoto na kutafutia ufumbuzi.


  Mlelwa amesema kuwa katika mwaka ujao wa fedha unaotarajia kuanza Julai Mosi 2024/2025 wakala huo umepanga kutekeleza Miradi 6 ya Maji sambamba na  kukamilisha ujenzi wa miradi ya maji  ya  Mbingu- Igima, na Mherule.

 

Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kilombero, mkoani Morogoro, Injinia Florence Mlelwa akizungumza na wadau wa mji.


“ Mwaka wa fedha 2024/2025 RUWASA Kilombero imepanga kutekeleza Miradi 6 ya Maji katika Vijiji vya
Mofu - Ihanga, Lugala, Nakaguru, Mgugwe – Chisano na Ngalimila sambamba na  Uchimbaji wa visima 10.

 

 Mlelwa alivitaja visima  vinavyotarajiwa kuchimbwa kuwa ni  kisima cha Ipinde, Lumumwe na  Ngalimila. Vingine ni  Ikwambi, Kalenga, Miyomboni,  Msita Ibaku, Iduindembo na Kitete.

 

Wadau wa maji wakifuatlia kwa makini taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji iliyotolewa na Meneja wa RUWASA wilaya ya Kilombero.

Anaongeza kusema kuwa  kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 Wilaya Kilombero inakadiriwa kuwa na watu 582,960, ikiwa watu 199,641 wapo katika eneo la Ifakara Mji ambao wanahudumiwa na Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira  (IFAUWASA) huku RUWASA inawahudumia watu 383,319 waishio vijijini ambao wanaopata maji safi na salama ni 297,838 sawa na asilimia 77.7%.


Akizungumza katika mkutano huo wa wadau wa maji, Mkuu wa Wilaya ya Kilomero, Dunstun Kyobya alipongeza kazi kubwa zinazofanywa na RUWASA wilayani humo, huku akiziagiza taasisi zote zinadaiwa bili za maji kulipa haraka ili kuiwezesha RUWASA kutekeleza majukumu yake kiufanisi.

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages