NA VICTOR MAKINDA, MOROGORO
SERIKALI imeipa
kipaumbele ajenda ya usalama wa chakula, ikizingatiwa dira ya kujilisha na
kuwalisha wengine kibiashara sambamba na kuhakikisha mipaka ya nchi inakuwa
wazi kwa kuuza chakula nje ikiwa ni mkakati wa kukamilisha mipango sita inayotokana na Mipango ya Maendeleo Endelevu
ya Milenia (SDGs) kwa lengo la kukomesha baa la njaa nchini kufikia mwaka 2030.
Mkurugenzi wa Masoko na Usalama wa Chakula kutoka Wizara ya Kilimo, Gungu Mibavu. |
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Masoko na Usalama wa Chakula kutoka Wizara ya Kilimo, Gungu Mibavu, kwenye mkutano wa wadau wa masuala ya usalama wa chakula (National Food system pathways roadmap and costed action plan) ulioandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kilimo na Cakula (FAO).
Mibavu alisema kuwa
mpaka sasa chakula kilichopo kinatosheleza
nchi na kubakiwa na ziada na kwamba hiyo inaonesha ni njia ya sahihi ya kufikia
malengo ya milenia yaliyokusudiwa.
Aliwataka
wadau wa mkutano huo kujidhatiti na kuhakikisha wanatumia vizuri miaka sita
iliyobakia ya kukamilisha malengo endelevu ya Maendeleo ya Milenia (SDGs) ya
mwaka 2030 waliyojiwekea tangu mwaka 2021.
Alisema tayari wameshakwisha
saini itifaki mbalimbali za kibiashara
kwenye kanda ikiwemo SADEC, EAC
inayohusu utekelezaji wa dira ya kujilisha wenyewe na kuwalisha wengine
kibiashara, kuongeza uzalishaji wa ndani wa chakula.
Naye Mratibu wa
Uhimilivu wa Mfumo ya Chakula kutoka Zanzibar, Sihaba Vuai, alisema katika kuhakikisha wanafanya mageuzi
ya kilimo wamejikita kwenye mifumo ya minyororo ya thamani 6 iliyopo kwenye
mazao ya kipaumbele.
Vuai ambaye pia ni
Mkurugenzi msadizi wa masuala ya sera aliyataja mazao hayo ya kipaumbele kuwa
ni pamoja na mazao ya kilimo, matunda, viungo, mifugo huku mkazo ukiwa ni kujikita katika
kuimarisha miundombinu ya uzalishaji katika kilimo cha umwagiliaji wa mpunga na
mazao ya mbogamboga.
Mratibu wa uhimilivu wa mifumo ya chakula kutoka Zanzibar Sihaba Vuai
Aliongeza kusema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kwa sasa ina
mpango wa kushirikisha serikali za mitaa katika masuala ya kilimo na kuwezesha
wilaya 10 kati ya 11 zilizopo Zanzibar kunufaika zaidi na kilimo.
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇