POLISI, TCRA WATOA NENO KWA
WAANDISHI WA HABARI MITANDAONI
Ripota, CCM Blog, Dar es Salaam
Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime, amewataka
waandishi wa habari za mtandaoni kufuata
sheria, kanuni na misingi ya habari wanapoandika kazi zao badala ya kuleta
uchochezi.
Aidha amesema, ulinzi na usalama wa Mwandishi wa habari ni
muhimu kwanza kuliko kitu kingine.
Akizungumza kwenye Kongamano la Jumuiya ya Wanahabari Mitandaoni (JUMIKITA), kwenye
Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam amesema, kuna kila sababu ya
mwandishi kuwa balozi wa amani, umoja na utulivu kwa kuchambua habari kabla ya
kuiandika.
Amesema waandishi wa habari wanatakiwa kuepuka habari za
uchochezi zinazovuruga amani ya nchi lakini lengo la mwandishi ni kupata
wasomaji wengi na kujikuta akiingia kwenye mgogoro na vyombo vya sheria.
Misime amesema: "Lazima
mzingatie Sheria mbalimbali za habari, msiandike habari tu kwa kuwa ni habari,
mkizingatia sheria, tutakuwa na mitandao mizuri itakayotupatia habari nzuri
katika jamii."
Ameutaka uongozi wa JUMIKITA kusaidia kutoa elimu kwa
wanahabari mtandaoni ili kudhibiti hali hiyo kama ambavyo Baraza la habari
Tanzania limekuwa likifanya.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano
Tanzania, TCRA, Mkurugenzi wa Leseni katika Mamlaka hiyo, John Daffa amesema
Tanzania ina watumiaji wa mitandao milioni 36 pamoja na vifaa ya kutumia
interneti milioni20.
Amesema tukitumia majukwaa haya ya habari vizuri pamoja na
mitandao kuna fursa nyingi ambazo zinaweza kuingiza kipato.
Daffa amesema kama wanahabari mtandaoni wanapaswa kuzingatia
usalama ikiwemo kutofungua link ambazo hawazifahamu sanjari na kutumia nywila
ambayo ni ngumu mtu mwingine kuifahamu kirahisi.

No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇