LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 3, 2023

OFISI YA MSAJILI WA HAZINA YANG’ARA, YAIBUKA YA KWANZA TUZO ZA NBAA

Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imeibuka mshindi wa kwanza katika tuzo za Uandaaji wa taarifa za fedha kwa mwaka 2023, katika kundi la Idara Huru za Serikali (Independent Government Department). Pichani, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Utendaji, Ufuatiliaji na Tathmini – Mashirika ya Kibiashara wa Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) Lightness Mauki, akikabidhiwa tuzo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, CPA Jamal Kassim Ally, wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo zilizondaliwa na Bodi ya Taifa ya Uhasibu na Ukaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki, Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Fedha na Uhasibu wa Taasisi hiyo Hassan Mohamed.

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages