Kimara, Dar es Salaam
Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango leo amekabidhi zawadi ambazo ni pamoja na vyakula, vinywaji, sabuni, mafuta ya kupikia na mavazi, katika Kituo cha kulea watoto yatima cha Jerusalem Home of God’s Love For Children kilichopo Kimara Jijini Dar es Salaam.
Akikabidhi zawadi hizo Msaidizi wa Makamu wa Rais masuala ya Sheria Elisha Suku amesema Makamu wa Rais ametoa zawadi hizo kusheherekea pamoja na watoto hao sikukuu za Krismasi na Mwaka mpya, huku akiwatakia heri na afya njema watoto pamoja na walezi wao.
Akipokea zawadi hizo, Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la KilutheriTanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani Usharika wa Kimara Jijini Dar es Salaam Wilbroad Matsai amemshukuru Makamu wa Rais kwa zawadi hizo pamoja na viongozi wote wanaojitolea kusaidia wenye uhitaji.
Your Ad Spot
Dec 23, 2023
Home
featured
KIJAMII
MAKAMU WA RAIS DK. MPANGO AWAPA SHANGWE YA KRISMAS NA MWAKA MPYA YATIMA JIJINI DAR ES SALAAM
MAKAMU WA RAIS DK. MPANGO AWAPA SHANGWE YA KRISMAS NA MWAKA MPYA YATIMA JIJINI DAR ES SALAAM
Tags
featured#
KIJAMII#
Share This
About CCM Blog
KIJAMII
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot


No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇