LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 13, 2023

MNEC SULTAN ATOA SHUKRANI KWA RAIS SAMIA KUIMWAGIA RUKWA FEDHA ZA MIRADI


 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa (NEC) kupitia Mkoa wa Rukwa, Sultan Saleh Seif ametoa shukrani kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuupatia Mkoa wa Rukwa Fedha lukuki za miradi ya maendeleo  Mkoa wa Rukwa.


Aidha ameiomba serikali kuupatia mkoa huo madaktari bingwa kutokana na upungufu mkubwa uliopop wa madakatari hao.


Ametoa shurani hizo na maombi hayo wakati wa mkutano wa kuhitimisha ziara ya siku nne ya Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Daniel Chongolo mkoani humo kwenye Uwanja wa Mandela mjini Sumbawanga Oktoba 11, 2023.


Ziara hiyo ya Chongolo ambaye aliambatana na Katibu wa NEC Oganaizesheni, Issa Haji Gavu ilikuwa ya kuimarisha uhai wa chama, kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua na kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025.

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 
MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM
 0754264203

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages