LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 15, 2023

TUMUENZI BABA WA TAIFA KWA KUWEKEZA KWENYE KILIMO CHA UMWAGILIAJI*



 14 Oktoba 2023, inatukumbusha mengi ambayo *Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere,* alitufanyia kwa lengo kuu la kuboresha uchumi na ustawi mzuri wa Taifa letu.


Baba wa Taifa alithamini sana kilimo na kuwekeza kwenye viwanda vya zana za kilimo (k.m. UFI), kiwanda cha mbolea, viwanda vya kutumia mazao yetu ya kilimo na ufugaji, vyuo vya kuzalisha wataalamu wa kilimo wa ngazi mbalimbali, vyama vya ushirika, ushirikiano na nchi za nje kwenye sekta ya kilimo, JKT yenye mashamba ya kilimo, tuzo na sherehe za wakulima.


Baba wa Taifa alipeleka nje ya nchi vijana wa ki-Tanzania kusomea masuala mbalimbali ya kilimo, ufugaji na uvuvi.


Vilevile, Baba wa Taifa aliamua kuwekeza kwenye kilimo kikubwa cha umwagiliaji na moja ya miradi hiyo ni ule wa Bonde la Bugwema la Musoma Vijijini.


Serikali imeamua kufufua Mradi wa Bugwema ambao miundombinu ya umwagiliaji ilianza kujengwa Mwaka 1974. Mradi ukasimama!


Tafadhali sikiliza CLIP/VIDEO kutoka Bonde la Bugwema, Musoma Vijijini - imeambatanishwa hapa.


Ofisi ya Mbunge

Jimbo la Musoma Vijijini

www.musomavijijini.or.tz 


Tarehe:

Jumamosi, tarehe 14.10.2023


No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages