LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 8, 2023

WAZEE WACHAPWA VIBOKO KATIKA MAKAO YA WAZEE KENYA

 


 Wakazi walio katika mazingira magumu katika makao ya wazee karibu na mji mkuu Kenya, Nairobi wamekuwa wakinyanyaswa na kutelekezwa, uchunguzi wa BBC Africa Eye umefichua.

Upigaji picha wa siri unaonyesha wafanyikazi wakiwatesa wakazi, wakitupa chakula moja kwa moja kwenye meza bila sahani yoyote, na kuwaacha bila matibabu.

"Mchape katika makalio. Mpige," mfanyikazi mmoja anamsihi mfanyakazi mwenzake aliyeshika fimbo, katika Kanisa la Presbyterian Church of East Africa (PCEA) Thogoto Care Home for the Aged, takriban kilomita 20 (maili 12) magharibi mwa Nairobi.

Picha za siri zinaonyesha kwamba muda mfupi kabla, wafanyakazi watatu waliovalia sare za rangi ya zambarau, wanamzingira mwanamke mzee karibu na lango la chuma lililozungukwa na mabati pembezoni mwa bustani ya nyumba hiyo.

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages