MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kibaha Mjini, Mwl. Mwajuma Nyamka ameagiza hatua za kisheria kuchukuliwa kwa viongozi wote wasio waadilifu bila kujali wana nyadhifa gani.
"Kiongozi anapaswa kuwa kimbilio, hivyo anapoonekana anawaumiza wananchi anapaswa kuchukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria kama ilivyo kwa mtu mwingine yeyote," alisema Mwl. Nyamka akiwa katika ziara ya kutembelea mabalozi katika kata ya Kibaha.
Mwl. Nyamka anasema CCM ni chama kilichoanzishwa kwa lengo la kusaidia jamii, sio kuwaumiza.
| Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Kibaha Mjini Clemence Kagaluki na Katibu wa UVCCM wilaya hiyo , Amina Makona |

No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇