Na Bashir Nkoromo, Mbezi Kwa Komba
Sanjari na Sherehe za Nane Nane, jana nyumbani kwa aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Marehemu Kapeni John Komba kulikuwa na hekaheka ya aina yake, ulipofanyika uzinduzi wa Shina la wakerekewa wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) tawi la Kapt. Komba, eneo la Tangibovu, Kawe jijini Dar es Salaam.
Kampteni Komba ambaye pia alikuwa Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi mkoani Ruvuma na na Mkurugenzi wa Bendi ya hamasa ya CCM, alifanriki dunia Jumamosi Februari 28, 2015, katika Hospitali ya TMJ, Jijini Dar es Salaam, ampako alipelekwa kupata matibabu baada ya kuugua akiwa nyumbani kwake.
Shina hilo ambalo Mwenyekiti wake ni Elias John Komba lilizinduliwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Kahama na Naibu Katibu Mkuu mstaafu Wizara ya Nishati Mhandisi Dk. Juliana Pallangyo na kukolezwa kwa sherehe iliyohitimishwa kwa kula na kusaza katika ukumbi wa Salome Social Hall unaomilikiwa na Mjene wa Marehemu Kapteni Komba ambaye pia ndiye mlezi wa Shina hilo la UVCCM.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Mhandisi Dk. Juliana aliwataka Vijana kuwa na umoja na kumlinda mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa anayofanya ya kukiimarisha Chama na kulijenga taifa.
Aliwataka Viajana hao kujituma katika kufanya kazi hasa za kujiajiri na wakati huohuo kuchangamkia mikopo inayotolewa na Rais Serikali ya Rais Samia kwa vijana, Kinamama na Wenye ulemavu kupitia halmashauri za Wilaya,
Mhandisi Dk. Juliana aliwapa moyo vijana kuwa atakuwa nao muda wote, ikiwa ni pamoja na kuwasaidia kwa yale yote ambayo yatakuwa ndani ya uwezo wake ambapo kwa kuanzia aliwaomba Kabla ya Jumapili wiki hii kukutana kwa wingi Salome Social Hall ili kujifunza ujasiriamali katika nyanja mbalimbali.
"Kuhusu ajira kama mlivyoomba katika risala yenu, hili siwezi kuwadanganya, maana nikijitahidi sana nitaajiri wawili au watatu tena mimi binafsi na haitakuwa ajira ya uhakika, maana nikiendewa vibaya nitawafukuza, sasa hii haitasaidia.
Hapa la msingi ni kuhakikisha mnafanya kazi za kujiajiri kupitia ujasiriamali, hivyo nawaomba ninyi mliokuja hapa leo kutoa mada za ujasiriamali, kabla ya Jumapili tukutane hapa na hawa vijana ili mtusaidie kuwafundisha kwa nafasi ya kutosha", alisema Mhandisi Dk. Juliana huku akimuagiza Mwenyekiti wa Shina Elias Komba kuhakikisha anawakusanya vijana ili wahudhurie kwa wingi mafunzo hayo.
Katika sherehe hiyo Mgeni rasmi pia alikabidhi jumla ya kadi 100 za UVCCM (50) na za CCM (50) kwa wanachama wapya. Walepewa pea mbili za kadi (za UVCCM na za CCM) ili kuweza kujisajili ki eletroniki kwa kuwa usajili wa kadi za Chama kwa njia hiyo haufanyiki kwa kwadi za Jumuiya.
Ufunguzi wa shina hilo la UVCCM ambao uliambatana na Mkutano Mkuu, ulihudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wakiwemo mlezi wa Shina Mama Salome Komba, Katibu wa CCM Kata ya Kawe Aisha Katundu, Katibu wa UVCCM Kata ya Kawe Neema Chisanga, Katibu wa Tawi la CCM la kampteni Komba Pili Busa na viongozi wengine kutoka matawi 12 ya CCM na UVCCM Kata hiyo ya Kawe.
Kampteni Komba ambaye alikuwa Mbunge wa Mbinga Mashariki alifanriki dunia Jumamosi Februari 28, 15
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Kahama, Naibu Katibu Mkuu mstaafu Wizara ya Nishati mstaafu Mhandisi, Dk. Juliana Pallangyo (katika vazi la njano) akisoma maelezo baada ya kuzindua shina hilo.Kisha akapandisha bendera
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Kahama, Naibu Katibu Mkuu mstaafu Wizara ya Nishati mstaafu Mhandisi, Dk. Juliana Pallangyo (katika vazi la njano) akisindkizwa na Mama Salome Komba (kushoto) kuingia ukumbini kuendelea na hafla ya uzinduzi shina hilo..
Katibu wa Hamasa wa Shina hilo Cde Adimu (Mtoto wa Mjumbe) akiongoza hafla hiyo.
Katibu wa Shina hilo Abdul Jamal Kitunguu akifanya utambulisho.
Mwenyekiti Elias Komba akisalimia baada ya kutambulishwa.
Katibu wa Hamasa na Chipukizi UVVCM kata ya Kawe akizungumza.
Katibu wa UVCCM Kata ya Kawe akizungumza.
Katibu Hamasa wa CCM Tawi la Kwa Kapt. Komba akizungumza.
Mwenyekiti Elias Komba akimkaribisha Katibu wa Tawi la CCM Kapt, Komba kuzungumza.
Katibu wa CCM Tawi la Kapt Komba Pili Busa akizungumza.
Mlezi wa Shina la UVCCM Kapt. Komba Mama Salome Komba akisalimia.
Muwezeshaji kutoka NMB akitoa mada
Mkufunzi wa ujasiriamali Coach Godfrey akitoa zawadi ya kitabu cha ujasiriamali kwa Mgeni rasmi Mhandisi Dk. Juliana.
Mkufunzi huyo akimpa kitabu cha ujasiriamali Mwenyekiti Elias Komba.
Mweneyekiti Elias Komba akizungumza, kisha akakabidhi mipira kwa vijana👇
Washiriki wakiwa ukumbini.
Meza kuu wakiwa wametulia kuangalia mambo yakienda vizuri. Kushoto ni Mama Komba na wapili ni Mwenyekiti Elias Komba.
Cde Kitunguu akisoma risala
Cde Kitunguu akikabidhi risala kwa mgeni rasmi.
Katibu wa CCM Kata ya Kawe akizunumza
Watoto mbalimbali ambao ni UVCCM wa baadaye wakiwa kwenye hafla hiyo
Mhandisi Dk. Juliana akizungumza.
Mwenyekiti Elias Komba akizungumza.
Baadhi ya viongozi wakiselebuka kumshangilia mwenyekiti Elias Komba baada ya kuzungumza.
Katibu Pili Busa akimkaribisha Mgeni rasmi kugawa kadi ya UVCCM na Chama
Mhandisi Dk. Juliana akikabidhi kadi ya UVCCM kwa mwanachama mpya.
Mhandisi Dk. Juliana akikabidhi kadi ya UVCCM kwa mwanachama mpya.Mhandisi Dk. Juliana akikabidhi kadi ya UVCCM kwa mwanachama mpya.
Mhandisi Dk. Juliana akikabidhi kadi ya UVCCM kwa mwanachama mpya.
Wawakilishi katika kukabidhiwa kadi wakila kiapo.
Mama Salome Komba akiomba Mungu akibariki chakula.
No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇