LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

May 5, 2023

RAIS DK. MWINYI AKABIDHIWA RIPOTI YA SENSA YA WATU NA KAZI, IKULU, ZANZIBAR, LEO

Ikulu, Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema  kupitia takwimu zilizotolewa na  Sensa  ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 Serikali ina jukumu la  kujipanga kwa utekelezaji wa kiuchumi na kijamii.


Ameyasema hayo leo Ikulu Zanzibar katika shughuli fupi ya kukabidhiwa ripoti ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 iliyofanywa na Makamu mwenza wa Kamati ya ushauri wa Sensa kitaifa , Makamu pili wa Rais Mhe.Hemed Suleiman Abdullah  na ujumbe wake .


Matokeo ya takwimu hizo  yameonesha kwamba ongezeko la idadi la Watu Zanzibar imefikia asilimia 3.7 kwa Mwaka.


Vilevile  ifikapo Mwaka 2025 kuhitimisha Dira ya Maendeleo ya Tanzania, Zanzibar itakuwa na idadi ya Watu wapatao Milioni 2.08  , Dunia  itakapohitimisha  malengo endelevu mwaka  2030 Zanzibar inakadiriwa idadi ya watu itakuwa milioni 2.44 , na mwisho wa Dira 2050 Zanzibar inakisiwa kuwa na idadi ya watu Milioni 4.63.



No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages