LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 2, 2023

ZIJUE NJIA MPYA ZA DALADALA KWENDA SOKO LA MACHINGA DODOMA


Eneo hili la kituo cha Daladala Machinga linatarajia kuhudumia takriban idadi ya Daladala zaidi ya 850 ambazo zitakuwa zikipita katika mizunguko ya mbalimbali.

 LATRA imeandaa utaratibu wa njia ambao Daladala zote zitafika hapo zikipita katika mizunguko iliyoandaliwa kama ifuatavyo:-


Daladala Zote zitakazotoka Maeneo ya Ihumwa, Nanenane,

Swawa, Udom na Benjamin Mkapa hospital zitapita

mzunguko wa Bohari, kuja Mzunguko wa uelekeo wa hospital

ya Mkoa, zitakuja mpaka eneo la Majengo kupita

Mshikamano, zitakuja mpaka mzunguko wa Barabara ya bahi

na kuingia hapa kituoni.


 Kisha zikishapakia abiria zitaondoka

hapo kupitia mzunguko wa uwanja wa ndege, zitapita eneo la

chako ni chako, zitapita Nyerere square kuja mzunguko wa

hospitali ya mkoa zinakata kushoto uelekeo wa barabara ya

Morogoro na kuendelea na safari zake.


 Daladala zitokazo eneo la Veyula, Msalato, St Gema na

Chang’ombe Juu zitakuja moja kwa moja mpaka mzunguko

wa barabara ya Bahi na kuingia kituoni hapa kisha

zitaendelea kupitia mzunguko wa uwanja wa ndege kupita

Chako ni Chako, Nyerere square, Mzunguko wa Hospital ya

Mkoa, Majengo sokoni, Mshikamano, Mzunguko wa Barabara

ya Bahi zitaingia hapa Machinga kuendelea kupakia abiria

kisha zitatoka na kuelekea uelekeo wa safari zake.


Pia Daladala zitokazo Nala, Mnada mpya na Nkuhungu

zitakuja moja kwa moja kuingia hapo kituoni, zitapita kuelekea

Mzunguko wa Uwanja wa Ndege, kuelekea Chako ni Chako,

Nyerere square, Mzunguko wa Hospital ya Mkoa, Majengo

sokoni, Mshikamano, Mzunguko wa Barabara ya Bahi

zitaingia hapo Machinga kuendelea kupakia abiria kisha

zitatoka na kuelekea uelekeo wa safari zake.


IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 
MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM 
0754264203

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages