LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 31, 2022

SIMULIZI LUKUKI ZA PELE KUHUSU USTADI, UTU WAKE AFRIKA

 


th

CHANZO CHA PICHA,ALAMY

Maelezo ya picha,

Pele alipozuru Kenya

Huku harakati za kuondoa ukoloni zikienea barani Afrika mwishoni mwa miaka ya 1950 na mwanzoni mwa miaka ya 1960, Pelé alialikwa na nchi mpya zilizokuwa huru kucheza mechi za kirafiki za kifahari na klabu yake ya Santos FC na timu ya taifa ya Brazil.

Katika wasifu wake, Pelé alisema kwamba miongo iliyofuata na safari za mara kwa mara katika bara la Afrika, "zilibadilisha sio tu mtazamo wangu wa ulimwengu, lakini pia jinsi ulimwengu ulivyonichukulia".

Mwandishi wa Almanac ya FC Santos, Guilherme Nascimento, alidokeza kwa usahihi kwamba safari za Kiafrika "zilijaa hadithi kiasi kwamba hakuna mpaka wazi kati ya hadithi na ukweli". 

Wakati wake huko Algeria, kwa mfano, ulikuwa kama simulizi ya  filamu.

Mnamo 1965, kijana huyo mwenye umri wa miaka 24 aliwasili wakati mkurugenzi wa filamu Gillo Pontecorvo alipokuwa akiunda filamu ya  The Battle of Algiers.

th

CHANZO CHA PICHA,ALAMY

Maelezo ya picha,

Pele alitembelea Kenya na Uganda katika miaka ya 1970

Kwa hivyo, ilikuwa kawaida kabisa kuona mizinga ya vita ikivuka Algiers kutoka katikati mwa jiji hadi Casbah.

Rais mpenda soka wa Algeria Ahmed Ben Bella alipanga mechi mbili za kirafiki kwa hafla hiyo - moja mjini Oran tarehe 15 Juni, na moja katika mji mkuu, Algiers, siku nne baadaye.

Hata hivyo, tarehe 17 Juni, Waziri wa Ulinzi wa Ben Bella Houari Boumediene alifanya mapinduzi, na kumuondoa rais madarakani na kufuta mechi ya pili.

Baadhi ya waandishi wa habari wanaoaminika na wanahistoria wanaamini kwamba Boumediene huenda alitumia mzozo uliokuwepo wakati wa kuwasili kwa Pele kama fursa  ili kutekeleza mapinduzi yake.

Unaweza pia kusoma
th

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Pele na nyota wa zamani wa Cameroon, Samuel Eto'o wakisalimiana na mashabiki katika mechi ya kumuenzi Nelson Mandela mwaka 2007.

Ziara nyingi za Pele nchini Morocco hazikuwa na msukosuko, lakini ni hadithi tu.

Ilisemekana kuwa alikuwa na maneno mazuri sana kwa wajumbe wa Morocco kwenye Kombe la Dunia la 1970 huko Mexico, kwani walikuwa taifa la kwanza la Kiafrika kufuzu kwa Kombe la Dunia tangu Misri mnamo 1934.

Katika safari nyingine, alidaiwa kuzungumza kuhusu Larbi Ben Barek, raia wa Morocco wa zama zake, ambaye alizichezea Olympique de Marseille na Atletico Madrid.

"Ikiwa mimi ndiye mfalme wa mpira wa miguu, basi Ben Barek ndiye mungu," alitangaza.

 

Vifuniko sita vya chupa kumuona Pele

Safari za Pele nchini Nigeria na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo pia zimegubikwa na hadithi.

Wakati wa safari zote mbili, alipewa sifa za kipekee  kwa kuleta amani katika nchi iliyokuwa mwenyeji wake.

Vita vya Wenyewe kwa Wenyewe vya Nigeria vilipamba moto kuanzia 1967-1970, lakini Pele alipotembelea nchi hiyo  mwaka 1969 kucheza mechi ya maonyesho dhidi ya timu ya taifa ya Nigeria, kulikuwa na madai kwamba usitishaji vita wa saa 48 ulikuwa umetangazwa.

"Sina uhakika ni kweli kabisa," Pelé alisema katika kitabu chake.

"Lakini Wanigeria kwa hakika walihakikisha Wabiafra hawangevamia Lagos tulipokuwa huko," alisema, akikumbuka uwepo mkubwa wa kijeshi. Hakukuwa na nafasi nyingi ya hilo kutokea ingawa, kama watenganishaji wa Biafra walikuwa angalau kilomita 500 (maili 310) na kusukumwa nyuma na jeshi.

Kufikia 1976, kampuni ya vinywaji baridi ya Marekani ya Pepsi ilitumia umaarufu wa Pele katika bara na kufadhili safari ya Afrika Mashariki kwenda Kenya na Uganda kwa nyota huyo mstaafu.

Huko, "The King" alifanikiwa kuuza kinywaji hicho na kuendesha kambi tofauti za kandanda kwa wachezaji wachanga katika nchi hizo mbili.

Nchini Kenya, mashabiki walipata kiingilio katika ukumbi huo kwa kuwasilisha vifuniko vya chupa za kinywaji hicho - sita kwa watu wazima, vitatu kwa watoto.

 

th

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Pele akiwa na Rais wa Gabon Ali Bongo katika uzinduzi wa sanamu yake mwaka 2012

Kwa miaka mingi, Pele pia alitembelea Msumbiji, Misri, Sudan, Senegal na Ghana.

Kando na ziara za hadhi ya juu, nembo ya Pele ilimaanisha mengi kwa wanasoka wanaochipukia kote barani Afrika.

"Nilipofika Ulaya, sisi Waafrika tulikuwa na Pelé, Mohamed Ali na Eusébio tu kama nyota wanaoonekana," alisema mwanasoka wa zamani wa Mali Salif Keita.

Mmoja wa wanasoka mashuhuri wa Ghana, Abedi "Pele" Ayew, hata alipewa jina la utani la nguli huyo wa soka wa Brazil.

"Binafsi, nilitiwa moyo sana na ukuu wake, na kufananishwa naye na kubeba jina lake la kitambo wakati wote wa kucheza na kuendelea, ni fursa nzuri na heshima kubwa," aliambia BBC.

Pelé mara zote alikuwa mtetezi wa maendeleo ya Afrika katika mashindano ya Kombe la Dunia la Fifa.

Utabiri wake katikati ya miaka ya 1970 kwamba timu ya Kiafrika ingeshinda shindano hilo kabla ya mwaka wa 2000 huwa ni mada motomoto kabla ya kila mchuano kuanza.

Inafaa  kukumbukwa kuwa chapisho lake la mwisho la mtandao wa kijamii lilijumuisha maneno machache ya pongezi kwa ajili ya michuano ya kihistoria ya Kombe la Dunia ya Morocco nchini Qatar.

"Singeweza kushindwa kuipongeza Morocco kwa kampeni ya ajabu. Ni vyema kuona Afrika inang'ara."

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages