LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 6, 2022

SHAKA: AZMA YA MWENYEKITI WA CCM RAIS SAMIA KUVIFANYIA MABORESHO YA KISASA ZAIDI VYOMBO VYA HABARI VYA CCM HAIPOI

CCM Lumumba, Dar es Salaam
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amesisitiza kwamba dhamira na azma ya Mwenyekiti wa CCM Rais Samia Suluhu Hassan ya kuvifanyia maboresho ya kimfumo na kiteknolojia vyombo vya habari vya CCM haijapoa na imeanza kufanyiwa kazi.

Amesema leo la Mwenyekiti wa CCM Rais Samia  kuvifanayia maboresho vyombo hivyo vya habari vya CCM ni kuhakikisha vinakidhi ipasavyo haja na mahitaji kulingana na mazingira ya wakati uliopo katika kuhabarisha umma.

Shaka amesisitiza hayo alipokuwa akizungumza na Viongozi na wafanayakazi wa vyombo hivyo katika kikao kilichofanayika leo, Jumamosi Agosti 6, 2022 katika ukumbi wa mikutano uliopo Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba, Jijini Dar es Salaam.

Amesema miongoni mwa hatua zilizoanza kuchukuliwa ni kuanza kwa mchakato wa kujengwa jengo ambalo ofisi za vyombo vyote vya habari vya CCM zitakuwa humo badala ya vyombo hivyo kufanyia kazi katika majengo ambayo vinalazimika kulipa kodi ya pango.

Shaka amesema lengo la ziara alizofanya katika baadhi ya vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini, pamoja na kujenga mahausiano mema, lakini pia ililenga kujifunza na kupata uzoefu ili Chama kiweze kusimamia vyema dhamira na azma ya Mwenyekiti wa CCM na Rais Samia katika kuvifanyia marekebisho na maboresho ya kimfumo vyombo vya chama ili vikidhi haja na mahitaji kulingana na mazingira ya wakati huu katika kuhabarisha umma.

“Hivi karibuni nilifanya  ziara katika baadhi ya vyombo vya habari vya serikali na binafsi ili kuimarisha mahusiano yetu lakini pia kujifunza na kupata uzoefu ili tuweze kusimamia vyema dhamira na azma ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Samia Suluhu Hassan katika kuvifanyia marekebisho na maboresho ya kimfumo vyombo vyetu vya chama ili vikidhi haja na mahitaji kulingana na mazingira ya wakati tulionao katika kuhabarisha umma” akasema Shaka.

Vyombo vya habari vya CCM ni Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Uhuru Publications Limited (UPL) Wachapishaji wa Magazeti ya Uhuru na Mzalendo na People's Media Communications Limited (PMCL) inayosimamia Kituo cha Radio cha Uhuru FM.

KATIBU wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka akizungumza nawafanyakazi wa  vyombo vya habari vya Chama  katika Ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Uhuru Publications Ltd (UPL) na Uhuru FM Shaaban Kisu akizungumza kabla ya Shaka kuzungumza na Wafanyakazi hao. Kushoto ni KaimuMkurugenzi wa RadioUhuru Amina Aziz
KATIBU wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka akizungumza na  Mkurugenzi Mkuu wa Channel Ten, Shaaban Kisu ambaye pia niKaimu Mkurugenzi Mkuu wa Uhuru Publications Limited na , People's  Media Communinication Limited (PMCL), wakati wa mkutano wake na wafanyakazi wa  vyombo vya habari vya Chama  katika Ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam leo.    
Shaka, Shaaban Kisu wakisikiliza kwa makini hoja za wafanyakazi Kushoto ni KaimuMkurugenzi wa Uhuru FM Amina Aziz. Shaka akinukuu hoja za wafanyakazi.👇👇👇




----------


Shaka akijibu hoja za wafanyakazi huku wafanyakazi wakimsikiliza kwa makini👇


No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages