Ikulu, Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali imepanga kuimarisha sekta ya bandari na sekta ya anga ili kukuza biashara ndani ya Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla.
Rais Samia amesema hayo leo wakati wa hafla ya ufunguzi wa Barabara ya Kikanda ya Afrika Mashariki (Arusha Bypass) yenye urefu wa kilomita 42.4. ambayo imegharimu shilingi Bilioni 197. 4.
Aidha, Rais Samia amesema barabara hii ni muhimu kwa nchi yetu kwa kuwa ni sehemu ya barabara kuu inayounganisha kanda ya Kaskazini (Northern Corridor) hadi Holili Taveta mpakani mwa Tanzania na Kenya kuelekea Voi nchini Kenya.
Barabara hii pia inaunganisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Tanga na Kanda mbalimbali zinazounganisha Tanzania na nchi jirani za Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Zambia Sudani Kusini na Sudani hadi Ethiopia.
Vile vile Rais Samia amesema kukamilika kwa barabara hii kumeimarisha sekta ya utalii pamoja na ukuaji wa uchumi na maendeleo ya kijamii katika mikoa inayopita, nchi kwa ujumla, pamoja na nchi jirani.
Your Ad Spot
Jul 22, 2022
Home
featured
Kitaifa
RAIS SAMIA: SERIKALI YA TANZANIA IMEJIPANGA KUIMRISHA SEKTA YA BANDARI NA ANGA ILI KUKUZA BISHARA AFRIKA
RAIS SAMIA: SERIKALI YA TANZANIA IMEJIPANGA KUIMRISHA SEKTA YA BANDARI NA ANGA ILI KUKUZA BISHARA AFRIKA
Tags
featured#
Kitaifa#
Share This
About Bashir Nkoromo
Kitaifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇